Thursday , 2 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Ratiba kuapishwa rais mpya Burundi yabadilishwa
Habari Mchanganyiko

Ratiba kuapishwa rais mpya Burundi yabadilishwa

Evariste Ndayishimiye, Rais wa Burundi
Spread the love

EVARISTE Ndayishimiye, rais mteule wa Burundi anatarajiwa kuapishwa kesho tarehe 18 Juni 2020, badala ya Agosti kama ilivyopangwa. Inaripoti mitandao ya kimataifa…(endelea).

Tume ya Uchaguzi ya Burundi wakati wa mchakato wa uchaguzi, ilileleza kwamba rais atakayechaguliwa na wananchi, ataabishwa Agosti, ratiba hiyo imebadilishwa baada ya kicho cha ghafla cha rais wa taifa hilo, Pierre Nkurunziza.

Imeelezwa, Ndayishimiye angeweza kuapishwa iwapo Nkurunziza angekuwa hai, lakini sasa nchi haina rais na si busara kusubiri wakati huo wakati hakuna kikwazo chochote kwa sasa.

Ndayishimiye anayetokana na chama tawala wa CNDD-FDD, ataapishwa katika Mji wa Gitega ikiwa ni wiki moja baada ya mtangulizi wake kufariki dunia kwa mshtuko wa moyo.

Nkurunziza alifariki dunia tarehe 8 Juni 2020. Baada ya kuapishwa, Ndayishimiye atahudumia taifa hilo kwa kipindi cha miaka saba.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Makonda autaka mgodi kubadilisha maisha ya wana-Geita

Spread the loveMKUU wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda ametoa wito kwa...

Habari MchanganyikoMakala & Uchambuzi

Je, miji ya Uingereza inafilisika?

Spread the loveMNAMO 1890, mwandishi mmoja wa habari Mmarekani aitwaye Julian Ralph...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Equity Bank yaendelea kusotea mabilioni ya fedha mahakama rufani

Spread the loveBENKI za Equity ya Tanzania na Kenya, zimeendelea kupambana mahakamani...

Habari Mchanganyiko

NEMC yatoa elimu matumizi sahihi ya zebaki kwa wachimbaji

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC)...

error: Content is protected !!