Friday , 19 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Ratiba kuapishwa rais mpya Burundi yabadilishwa
Habari Mchanganyiko

Ratiba kuapishwa rais mpya Burundi yabadilishwa

Evariste Ndayishimiye, Rais wa Burundi
Spread the love

EVARISTE Ndayishimiye, rais mteule wa Burundi anatarajiwa kuapishwa kesho tarehe 18 Juni 2020, badala ya Agosti kama ilivyopangwa. Inaripoti mitandao ya kimataifa…(endelea).

Tume ya Uchaguzi ya Burundi wakati wa mchakato wa uchaguzi, ilileleza kwamba rais atakayechaguliwa na wananchi, ataabishwa Agosti, ratiba hiyo imebadilishwa baada ya kicho cha ghafla cha rais wa taifa hilo, Pierre Nkurunziza.

Imeelezwa, Ndayishimiye angeweza kuapishwa iwapo Nkurunziza angekuwa hai, lakini sasa nchi haina rais na si busara kusubiri wakati huo wakati hakuna kikwazo chochote kwa sasa.

Ndayishimiye anayetokana na chama tawala wa CNDD-FDD, ataapishwa katika Mji wa Gitega ikiwa ni wiki moja baada ya mtangulizi wake kufariki dunia kwa mshtuko wa moyo.

Nkurunziza alifariki dunia tarehe 8 Juni 2020. Baada ya kuapishwa, Ndayishimiye atahudumia taifa hilo kwa kipindi cha miaka saba.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

Habari Mchanganyiko

Carbon First, Ruangwa wasaini makubaliano ya biashara ya hewa ukaa

Spread the love  KAMPUNI ya Carbon First Tanzania Limited na Halmashauri ya...

Habari Mchanganyiko

CBE yawakumbuka wenye mahitaji maalum Jangwani

Spread the loveCHUO cha Elimu ya Biashara (CBE), kimetoa msaada mbalimbali na...

Habari Mchanganyiko

Mume auwa mke kwa kumchoma visu, ajisalimisha Polisi

Spread the loveJACKSON Kalamji (49), anashikiliwa na Jeshi la Polisi jijini Mwanza,...

error: Content is protected !!