Wednesday , 8 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Awamu ya Tano: Watumishi 32,555 ‘waisoma namba’
Habari za Siasa

Awamu ya Tano: Watumishi 32,555 ‘waisoma namba’

Seleman Jafo
Spread the love

JUMLA ya watumishi 32,555 wamechukuliwa hatua mbalimbali za kinidhamu ikiwemo kufukuzwa kazi, kushushwa vyeo na kushushwa mishahara katika serikali inayoongozwa na Rais John Magufuli. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Waliokutwa na dhoruba hizo ni wale waliobainika kuwa wazembe kazini, kughushi vyeti, rushwa na matumizi mabaya ya madaraka.

Kauli hiyo imetolewa na Rais John Magufuli leo Jumanne tarehe 16 Juni 2020, bungeni jijini Dodoma, katika hafla ya ufungaji wa shughuli za Bunge la 11.

“Kama tulivyoahidi, hatutakuwa na mzaha kwa viongozi na watumishi wazembe walioshindwa kufanya kazi kwa weledi, nidhamu, maalifa na uadilifu. Waliobainika walichukuliwa hatua za kinidhamu ikiwemo kuwatumbua, kuwashusha vyeo na mishahara au kuwapa onyo kali,” amesema Rais Magufuli.

Rais wa Tanzania, John Magufuli

Kiongozi huyo wa Tanzania amesema, katika uongozi wake, watumishi 15,508 waliachishwa kazi baada ya kukutwa na vyeti vya kughushi, alifuta ajira hewa 19,708 zilizokuwa zikigharimu Sh. 19.8 bilioni na kwamba, hatua hiyo ilitoa fursa ya kaujiri watumishi wapya 74,173.

Pia amesema, serikali yake imefanikiwa kuwapandisha vyeo watumishi 306,967 na kulipa madeni mbalimbali ya watumishi kiasi cha Sh. 472.6 Bil., ambapo ya kimshahara ni Sh. 114.5 Bil., na yasiyo ya kimshahara Sh. 358.1 Bil.

Serikali ya Rais Magufuli alianza kuongoza Tanzania Novemba 2015. Serikali imetambulika zaidi kwa mtindo wa ‘kutumbua’ watumishi walioonekana kutokwenda sawia na mwendo wa serikali hiyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Rais Samia ni Mzanzibari: Shida Iko Wapi?

Spread the loveTAIFA linakabiliwa na upungufu wa fikra sahihi. Upungufu huu unaonekana...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Mpina mwiba CCM, ahofia kuzibwa mdomo

Spread the loveWAKATI Chama cha Mapinduzi (CCM), kikijinasibu kuwa kinara wa demokrasia...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Mabeyo ametuepusha

Spread the loveNIMEGUSWA na uadilifu, utiifu na uaminifu wa Mkuu mstaafu wa...

Habari za SiasaTangulizi

CCM yaitaka TAKUKURU kuichunguza Chadema tuhuma alizoibua Lissu

Spread the loveCHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimeitaka Taasisi ya Kuzuia na Kupambana...

error: Content is protected !!