Tuesday , 7 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Spika Ndugai: Dodoma ni salama, hakuna tatizo
Habari za Siasa

Spika Ndugai: Dodoma ni salama, hakuna tatizo

Spika wa Bunge, Job Ndugai
Spread the love

JOB Ndugai, Spika wa Bunge la Tanzania amevitaka vyombo vya dola nchini humo kutoa haraka taarifa za awali za uchunguzi wa tukio la kushambuliwa kwa Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea)

Spika Ndugai ametoa kauli hiyo leo Jumanne tarehe 9 Juni 2020 bungeni jijini Dodoma, wakati akiwaeleza wabunge hali ya Mbowe baada ya kutoka kumwona katika Hospitali aliyokuwa amelazwa kabla ya kuhamishiwa jijini Dar es Salaam kwa matibabu.

Amesema, wakati anakwenda kumwona, amemkuta Mbowe ambaye ni Mwenyekiti wa Chadema akinywa chai na hali yake inaendelea vizuri huku akisema, hawezi kuongea zaidi kuhusu tukio hilo kwa madai lina mazingira yenye utata yanayoweza kuwekwa wazi na polisi.

Spika Ndugai amevitaka vyombo vya dola kuharakisha kutoa taarifa za uchunguzi wa tukio hilo ili kuepuka kuzusha maneno yasiyokuwa na maana kuhusu tukio hilo, “vyombo vya ulinzi na usalama vitoke mapema viseme nini kimetokea.”

Freeman Mbowe, Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni alisafirishwa kutoka Dodoma kwenda Dar es Salaam kwa matibabu zaidi

“Naamini kesho (Jumatano) jioni saizi, nitakuwa na kiasi fulani cha kusema,” amesema Spika Ndugai

Akiendelea kuzungumza, Spika Ndugai amesema, hali ya usalama Dodoma haujatetereka.

“Niwahakikishie waheshimiwa wabunge, Dodoma ni salama, salama kabisa kabisa. Mmekaa hapa toka Aprili mwanzoni hadi sasa, hakuna aliyepoteza sikio, jicho, aliyechomoka mkono au kidole. Dodoma ni salama,” amesema Spika Ndugai

1 Comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Rais Samia ni Mzanzibari: Shida Iko Wapi?

Spread the loveTAIFA linakabiliwa na upungufu wa fikra sahihi. Upungufu huu unaonekana...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Mpina mwiba CCM, ahofia kuzibwa mdomo

Spread the loveWAKATI Chama cha Mapinduzi (CCM), kikijinasibu kuwa kinara wa demokrasia...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Mabeyo ametuepusha

Spread the loveNIMEGUSWA na uadilifu, utiifu na uaminifu wa Mkuu mstaafu wa...

Habari za SiasaTangulizi

CCM yaitaka TAKUKURU kuichunguza Chadema tuhuma alizoibua Lissu

Spread the loveCHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimeitaka Taasisi ya Kuzuia na Kupambana...

error: Content is protected !!