Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Spika Ndugai: Dodoma ni salama, hakuna tatizo
Habari za Siasa

Spika Ndugai: Dodoma ni salama, hakuna tatizo

Spika wa Bunge, Job Ndugai
Spread the love

JOB Ndugai, Spika wa Bunge la Tanzania amevitaka vyombo vya dola nchini humo kutoa haraka taarifa za awali za uchunguzi wa tukio la kushambuliwa kwa Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea)

Spika Ndugai ametoa kauli hiyo leo Jumanne tarehe 9 Juni 2020 bungeni jijini Dodoma, wakati akiwaeleza wabunge hali ya Mbowe baada ya kutoka kumwona katika Hospitali aliyokuwa amelazwa kabla ya kuhamishiwa jijini Dar es Salaam kwa matibabu.

Amesema, wakati anakwenda kumwona, amemkuta Mbowe ambaye ni Mwenyekiti wa Chadema akinywa chai na hali yake inaendelea vizuri huku akisema, hawezi kuongea zaidi kuhusu tukio hilo kwa madai lina mazingira yenye utata yanayoweza kuwekwa wazi na polisi.

Spika Ndugai amevitaka vyombo vya dola kuharakisha kutoa taarifa za uchunguzi wa tukio hilo ili kuepuka kuzusha maneno yasiyokuwa na maana kuhusu tukio hilo, “vyombo vya ulinzi na usalama vitoke mapema viseme nini kimetokea.”

Freeman Mbowe, Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni alisafirishwa kutoka Dodoma kwenda Dar es Salaam kwa matibabu zaidi

“Naamini kesho (Jumatano) jioni saizi, nitakuwa na kiasi fulani cha kusema,” amesema Spika Ndugai

Akiendelea kuzungumza, Spika Ndugai amesema, hali ya usalama Dodoma haujatetereka.

“Niwahakikishie waheshimiwa wabunge, Dodoma ni salama, salama kabisa kabisa. Mmekaa hapa toka Aprili mwanzoni hadi sasa, hakuna aliyepoteza sikio, jicho, aliyechomoka mkono au kidole. Dodoma ni salama,” amesema Spika Ndugai

1 Comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!