Tuesday , 30 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Ofisa Takukuru ‘feki’ abambwa kwa kujipatia Sh. 90,000
Habari Mchanganyiko

Ofisa Takukuru ‘feki’ abambwa kwa kujipatia Sh. 90,000

Pingu
Spread the love

JAFET Emmanuel, Mkazi wa Kilimahewa katika Manispaa ya Kigoma Ujiji, anashikiliwa na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), kwa kosa la kupata fedha kwa njia za udanganyifu. Anaripoti Mwandishi Wetu, Kigoma … (endelea).

Taarifa iliyotolewa leo Ijumaa tarehe 5 Juni 2020 na Nestory Gatahwa, Naibu Mkuu wa TAKUKURU mkoa wa Kigoma imesema Emmanuel alijifanya afisa wa Takukuru kisha kutumia cheo hicho cha kughushi, kuomba fedha baadhi ya wananchi, waliokuwa wanahitaji huduma kwenye taasisi hiyo.

Katika tukio la kwanza, Emmanuel anadaiwa kuomba rushwa ya Sh. 300,000 kutoka kwa mwananchi, aliyemuahidi anaweza kutengua maamuzi ya mahakama dhidi ya shauri la mgogoro wa shamba alilokuwa nalo.

“Katika kufanikisha nia yake ovu, mtuhumiwa amejipatia Sh. 90,000 kutoka kwa mwananchi, ikiwa ni sehemu ya fedha Sh. 300,000, ambazo mtuhumiwa alimweleza mwananchi huyo ni fedha kwa ajili ya kuwezesha kutenguliwa kwa maamuzi ya mahakama katika shauri alilokuwa nalo,” inaeleza taarifa ya Gatahwa.

Tukio la pili, Emmanuel anadaiwa kuomba rushwa ya Sh. 500,000 kutoka kwa mwananchi, ili amsaidie kupata kazi katika ofisi za Takukuru. Hata hivyo, mwananchi huyo hakutoa kiasi hicho cha fedha.

Gatahwa amesema uchunguzi dhidi ya mtuhumiwa huyo unaendelea na kwamba atafikishwa mahakamani mara baada ya uchunguzi na taratibu nyingine za kisheria kukamilika.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

7 wafa Ulanga, mbunge alia kutelekezwa na mawaziri, Tanroad

Spread the loveWatoto saba wamepoteza maisha na zaidi ya kaya 70 kukosa...

Habari Mchanganyiko

Bil 12.4 zimetumika ujenzi wa miradi wilaya ya Momba

Spread the love MKUU wa wilaya ya Momba mkoani Songwe Kennan Kihongosi...

AfyaHabari Mchanganyiko

Songwe katika mikakati ya elimu ya lishe kudhibiti udumavu

Spread the love  SERIKALI mkoani Songwe imejipanga kuendelea kutoa elimu ya lishe...

Habari Mchanganyiko

NBC yapata tuzo ya mwezeshaji bora wa mikopo serikali Afrika

Spread the loveBenki ya NBC imepata tuzo ya Mwezeshaji Bora wa Pamoja...

error: Content is protected !!