Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Vurugu mkutano wa Waitara, Meya  jiji la Mwanza alazwa rumande
Habari za Siasa

Vurugu mkutano wa Waitara, Meya  jiji la Mwanza alazwa rumande

James Bwire, Meya wa Jiji la Mwanza
Spread the love

POLISI Mkoa wa Mwanza nchini Tanzania, limemkamata na kumhoji, Meya wa Jiji la Mwanza, James Bwire kwa tuhuma zinazomkabili. Anaripoti Mwandishi Wetu, Mwanza … (endelea).

Bwire ambaye ni Diwani wa Mahina kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM), anatuhumiwa kuandaa kikundi cha watu, waliovuruga mkutano wa Naibu Waziri wa Tamisemi, Mwita Waitara alioufanya katika moja ya kata za Jiji hilo tarehe 27 Mei, 2020.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Jumanne Muliro akizungumza na waandishi leo Jumamosi tarehe 30 Mei, 2020 amesema, walimkamata jana jioni Meya Bwire na kumhoji kwa saa 4 kisha wakamalaza rumande.

“Baada ya kuwa hapatikana kwa urahisi, askari polisi ambao moja ya jukumu lao kumfuata na akaletwa jana jioni kwa mahojiano kulingana na tuhuma nzito ambazo sisi tulizipata.”

Mwita Waitara, Naibu Waziri wa Ofisi ya Rais-TAMISEMI

“Ni kweli alishikiriwa na kwamba tarehe 27 Mei 2020, Naibu waziri wa Tamisemi (Mwita) alifanya kikao katika moja ya Kata jiji la Mwanza na zikapatikana taarifa meya wa jiji hili, aliandaa kikundi cha watu ambacho kikao kinafanyika, kilifanya fujo, kikatoa maneno ya kashfa na kejeli dhidi ya waziri na Serikali na kusababisha kuvunjika kwa kikao kile,” amesema

Amesema, kutokana na tuhuma zito, walimhoji kwa saa nne na kutokana na mazingira, alipumzishwa na kuendelea tena kwa mahojiano hadi alipomaliza leo na kuachiwa kwa dhamana.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

error: Content is protected !!