Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Vurugu mkutano wa Waitara, Meya  jiji la Mwanza alazwa rumande
Habari za Siasa

Vurugu mkutano wa Waitara, Meya  jiji la Mwanza alazwa rumande

James Bwire, Meya wa Jiji la Mwanza
Spread the love

POLISI Mkoa wa Mwanza nchini Tanzania, limemkamata na kumhoji, Meya wa Jiji la Mwanza, James Bwire kwa tuhuma zinazomkabili. Anaripoti Mwandishi Wetu, Mwanza … (endelea).

Bwire ambaye ni Diwani wa Mahina kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM), anatuhumiwa kuandaa kikundi cha watu, waliovuruga mkutano wa Naibu Waziri wa Tamisemi, Mwita Waitara alioufanya katika moja ya kata za Jiji hilo tarehe 27 Mei, 2020.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Jumanne Muliro akizungumza na waandishi leo Jumamosi tarehe 30 Mei, 2020 amesema, walimkamata jana jioni Meya Bwire na kumhoji kwa saa 4 kisha wakamalaza rumande.

“Baada ya kuwa hapatikana kwa urahisi, askari polisi ambao moja ya jukumu lao kumfuata na akaletwa jana jioni kwa mahojiano kulingana na tuhuma nzito ambazo sisi tulizipata.”

Mwita Waitara, Naibu Waziri wa Ofisi ya Rais-TAMISEMI

“Ni kweli alishikiriwa na kwamba tarehe 27 Mei 2020, Naibu waziri wa Tamisemi (Mwita) alifanya kikao katika moja ya Kata jiji la Mwanza na zikapatikana taarifa meya wa jiji hili, aliandaa kikundi cha watu ambacho kikao kinafanyika, kilifanya fujo, kikatoa maneno ya kashfa na kejeli dhidi ya waziri na Serikali na kusababisha kuvunjika kwa kikao kile,” amesema

Amesema, kutokana na tuhuma zito, walimhoji kwa saa nne na kutokana na mazingira, alipumzishwa na kuendelea tena kwa mahojiano hadi alipomaliza leo na kuachiwa kwa dhamana.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!