Monday , 6 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Magufuli awaapisha viongozi sita Dodoma
Habari za Siasa

Rais Magufuli awaapisha viongozi sita Dodoma

Spread the love

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, John Pombe Magufuli leo Alhamisi tarehe 21 Mei 2020 amewaapisha viongozi sita aliowateua hivi karibuni. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Hafla ya kuwaapisha viongozi hao imefanyika katika Ikulu ya Chamwino jijini Dodoma asubuhi hii.

Viongozi walioapishwa ni; Dk. Godwin Mollel kuwa Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii,Jinsia Wanawake Wazee na Watoto.

Dk. Mollel ameapishwa kuchukua nafasi ya Dk. Faustine Ndungulile ambaye uteuzi wake ulitenguliwa.

Dk. Delphine Magere ameapishwa kuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Pwani kuchukua nafasi ya Theresia Mbando ambaye amestaafu kwa mujibu wa utumishi wa umma.

Wengine ni; Dk. Jacob Kingu kuwa Balozi wa Tanzania nchini Algeria, Phaustine Kasike kuwa Balozi wa Tanzania nchini Msumbiji na John Simbachawene kuwa Balozi wa Tanzania nchini Kenya.

Pia, Rais Magufuli amemwapisha Brigedia Jenerali, John Mbungo kuwa Mkurugenzi mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na kupambana na Rushwa (Takukuru).

Hafla hiyo imehudhuriwa na viongozi mbalimbali wakiwamo mawaziri na wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama.

Endelea kufuatilia MwanaHALISI ONLINE kwa habari zaidi 

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Jacob, Malisa wapandishwa kizimbani kwa mashtaka ya uongo mitandaoni

Spread the loveMKURUGENZI wa Shirika la Haki, Godlisten Malisa na mwanachama wa...

BiasharaHabari za Siasa

Bunge laitaka Serikali kudhibiti ufisadi miradi ya mkakati

Spread the loveKAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, imeitaka Serikali kuimarisha...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Wizara ya Uchukuzi yaomba kuongezewa bajeti na Bunge

Spread the loveWIZARA ya Uchukuzi imeliomba Bunge liidhinishe bajeti yake kwa mwaka...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Serikali kutafuta mwekezaji mwingine Bandari ya Dar es Salaam

Spread the loveSERIKALI inaendelea kutafuta mwekezaji mwingine atakayeendesha gati namba nane hadi...

error: Content is protected !!