HAMIM Gwiyama, Mkuu wa Wilaya (DC) wa Nyang’hwale mkoani Geita amefariki dunia. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam…(endelea).
Taarifa iliyotolewa na Rebecca Kwandu, Mkuu wa KItengo cha Mawasiliano wa Ofisi ya Rais- Tamisemi imemnukuu Waziri wa Tamisemio, Seleman Jafo akitangaza kifo cha Gwiyama kilichotokea leo Alhamisi tarehe 7 Mei 2020 saa 5 asubuhi katika Hospitali ya Rufaa Bugando baada ya kuugua kwa muda mfupi.
Waziri Jafi amesema DC huyo aliongoza wizara hiyo tangu tarehe 26 Juni 2016 alipoteuliwa na Rais John Pombe Magufuli.
Katika taarifa hiyo, Waziri Jafo amemtumia salamamu za rambirambi mkuu wa mkoa wa Geita, Robert Gabriel, wananchi wa wilaya hiyo, ndugu, jamaa na wote walioguswa na msiba huo.
Kifo cha Gwiyama kimetokea ikiwa ni takribani siku kumi tangu Evod Mmanda, aliyekuwa
Mkuu wa Wilaya ya Mtwara kufariki dunia, tarehe 27 Aprili 2020.
Leave a comment