Tuesday , 30 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Magufuli afanya uteuzi wa RAS, DC
Habari za Siasa

Rais Magufuli afanya uteuzi wa RAS, DC

Rais John Magufuli
Spread the love

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, John Pombe Magufuli amemteua Dk. Delphine Magere kuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Pwani (RAS). Aanaripoti Mwandshi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Dk. Magere anachukua nafasi ya Theresia Mmbando ambaye amestaafu.

Taarifa iliyotolewa leo Jumatano tarehe 6, 2020 na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, Gerson Msigwa imesema kabla ya uteuzi huo, Dk. Magere alikuwa Ofisi ya Rais akishughulikia masuala ya uchumi.

Wakati huo huo, Rais Magufuli amemteua Dunstan Kyobya kuwa Mkuu wa Wilaya ya Mtwara (DC), mkoani Mtwara.

Kyobya anachukua nafasi ya Evod Mmanda aliyefariki Dunia tarehe 27 Aprili, 2020.

Kabla ya uteuzi huo, Kyobya alikuwa Mshauri wa Rais katika masuala ya sheria.

Uteuzi wa viongozi hao unaanza leo tarehe 06 Mei, 2020.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

Habari za SiasaTangulizi

Samia ataja miradi ambayo Tanzania inashirikiana na IDA

Spread the loveRais wa Tanzania Dk. Samia Suluhu Hassan leo Jumatatu amehutubia...

error: Content is protected !!