Thursday , 2 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Dawa ya corona kutua Tanzania
Habari Mchanganyiko

Dawa ya corona kutua Tanzania

Spread the love

DAWA ya ugonjwa wa corona (COVID-19), inayotengeneza nchini Madagascar, sasa itatumika nchini Tanzania. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam…(endelea).

Ni kwa kuwa, Serikali ya Tanzania ina mpango wa kupeleka ndege yake nchini humo kwa ajili ya kubeba na kuleta nchini dawa hiyo, ili kutibu wananchi wake.

Rais John Magufuli ametoa kauli hiyo leo tarehe 3 Mei 2020, wakati akimwapisha Mwigulu Nchemba, Waziri wa Katiba na Sheria.

Mwigulu amechukua nafasi ya Balozi Dk. Augustine Mahiga aliyefariki dunia tarehe 1 Mei 2020 mjini Dodoma. Dk. Mahiga amezikwa jana nyumbani kwao Tosamaganga, Iringa. 

Rais Magufuli amesema,  Madagascar imeiandikia barua Tanzania kuhusu  dawa hiyo, na kwamba Tanzania imeona ni muhimu kuchukua dawa hiyo na kuileta nchini kwa ajili ya kuwasaidia Watanzania.

“Nimewasiliana na watu wa Madagascar, kuna dawa kule ya corona wanasema wameipata, nitatuma ndege hiyo dawa ije hapa tuitumie,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

NEMC yatoa elimu matumizi sahihi ya zebaki kwa wachimbaji

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC)...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Oryx gesi yagawa mitungi, majiko 100 kwa waandishi wa habari Dar

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gesi Tanzania imegawa mitungi 100 ya gesi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

error: Content is protected !!