Wednesday , 8 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Kanisa la Mlima wa Moto watangaza wiki ya maombelezo
Habari Mchanganyiko

Kanisa la Mlima wa Moto watangaza wiki ya maombelezo

Mch. Getrude Lwakatare
Spread the love

MCHUNGAJI Kiongozi wa Kanisa la Mlima wa Moto lililopo Sabasaba Jijini Dodoma, Slivanus Komba ametangaza maombi ya Maombolezo ya siku saba ikiwa ni sehemu ya kumuenzi Dk. Getrud Rwakatale. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).

Mchungaji Komba ambaye pia ni Askofu wa Kanda ya Kati na  Nyanda za Juu kusini amesema lengo la maombolezo hayo ni kumuenzi kwa vitendo kutokana na mema na maonyo alikuwa akiyatenda mbeba maono wa Kanisa hilo na aliyekuwa askofu mkuu wa Kanisa la Mlima wa Moto Tanzania, Marehemu Mch. Rwakatale.

Askofu Komba alisema pamoja na kutangaza maombolezo ya siku saba ya Kanisa hilo pia litaendelea na maombolezo ya siku 40 ambayo yametangazwa kitaifa na Kanisa hilo ambayo yatakuwa ya kitaifa.

Kiongozi huyo wa Kiroho alisema kuwa kibiblia hakuna kioongozi yeyoye wa kidini ambaye anaweza kufanya maombolezo kwa ajili ya kumshawishi Mungu kubadilisha mawazo ya mtu aliyekufa kumpeleka peponi au motini kulingana na kile ambacho alikitenda akiwa hai.

Alisema wakati wa uhai wa Mch. Dk. Rwakatale alikuwa ni mstari wa mbele katika kuhakikisha kazi ya Mungu inasonga mbele licha ya kuwa alikuwa mfanyabiashara mkubwa na mwanasiasa.

Katika ibada hiyo ambayo ilikuwa ya tofauti ambayo ilighubikwa na majonzi vilio kwa washirika wa kanisa hilo, Askofu Komba aliwataka waumini wote kuhakikisha wanahudhuria Ibada zote za siku bila kukosa ikiwa ni sehemu ya maombolezo.

Katika hatua nyingine, Askofu Komba amekemea baadhi ya uzushi juu ya wanaopakaza kuhusu mrithi wa Mchungaji Kiongozi wa Kanisa hilo.

“Pamoja na kuwa Mimi siyo msemaji wa Kanisa hili wapo wasemaji lakini nipende kusema kuwa kwa sasa tupo katika kipindi kigumu cha kuondokewa na Kiongozi wetu mbeba maono.

“Nashangaa kwa mtu yeyote ambaye anawaza kurithi sisi hatupo kwa ajili ya kurithi, tunawaza kufanya kazi ya Mungu na kwa sasa Kanisa lipo ya Baraza la wazee.

“Kwa mtu ambaye anawaza kurithi hana nia njema na huduma ya kuifanya kazi ya Mungu bali maamuzi yote yatatolewa na Baraza la wazee wa kanisa baada ya siku 40,” alisema Askofu Komba.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Rais Samia: Matumizi ya nishati safi sio anasa, ladha ipo

Spread the loveRAIS Samia Suluhu Hassan amesema matumizi ya nishati safi kwa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC, SILABU waungana kufikisha elimu ya fedha majumbani

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) imeingia makubaliano ya ushirikiano...

AfyaHabari MchanganyikoMakala & Uchambuzi

Kisukari cha mimba ni nini?

Spread the loveKisukari cha mimba ni aina ya kisukari kinachotokea kwa baadhi...

Habari Mchanganyiko

Mafunzo kwa bodaboda 395 yamkuna Meya Dodoma

Spread the loveNAIBU Meya wa Jiji la Dodoma, Asma Karama amepongeza mafunzo...

error: Content is protected !!