Sunday , 28 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Magufuli: Uchaguzi Mkuu palepale
Habari za Siasa

Rais Magufuli: Uchaguzi Mkuu palepale

John Magufuli, Rais wa Tanzania
Spread the love

LICHA ya kuwepo kwa tishio la kusambaa kwa virusi vya corona (COVID-19) nchini, uchaguzi mkuu unaoratajiwa kuwanyika Oktoba mwaka huu, hautaahirishwa. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).

Akizungumza jijini Dodoma leo tarehe 26 Machi 2020, Rais John Magufuli amesema, uchaguzi huo hautasogweza mbele, kwa kuwa hakuna mtu anayetaka kuendelea kukaa madarakani.

Ametoa kauli hiyo huku kukiwa na taarifa zisizothibitishwa kwamba, uchaguzi huo utafanyika mwaka 2021 kutokana na tishio la ugonjwa corona.

“Hatujazuiliwa kukutana, sisi tunaendelea kukutana na tunakutana katika mikutano ya kawaida, na uchaguzi tutafanya tu, wako wengine wanafikiri nitaahirisha, nani anataka kukaa kwenye maofisi muda wote huo?” amehoji Rais Magufuli.

Rais Magufuli amesema, kazi zitaendelea kufanyika ikiwemo vikao vya bunge vitaendelea.

“Hatujazuiliwa kukutana, leo nilikuwa nasoma gazeti moja linasema Madiwani wafanya kikao sijui alifikiri wamezuiliwa kukutana kwa sababu ya Corona? Sisi tunaendelea kukutana, hata nchi zilizoathirika, bado mabunge na mabaraza hayajafungwa,”amesema Rais Magufuli.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde aibana kampuni kutimiza masharti ya mkataba

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameitaka Kampuni ya Xin Tai...

Habari za Siasa

Sauti ya Watanzania waeleza sababu za kuiunga mkono Chadema

Spread the love  KIKUNDI kinachojipambanua katika kupigania rasilimali na uhuru wa nchi,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

error: Content is protected !!