Tuesday , 3 October 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Magufuli: Uchaguzi Mkuu palepale
Habari za Siasa

Rais Magufuli: Uchaguzi Mkuu palepale

John Magufuli, Rais wa Tanzania
Spread the love

LICHA ya kuwepo kwa tishio la kusambaa kwa virusi vya corona (COVID-19) nchini, uchaguzi mkuu unaoratajiwa kuwanyika Oktoba mwaka huu, hautaahirishwa. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).

Akizungumza jijini Dodoma leo tarehe 26 Machi 2020, Rais John Magufuli amesema, uchaguzi huo hautasogweza mbele, kwa kuwa hakuna mtu anayetaka kuendelea kukaa madarakani.

Ametoa kauli hiyo huku kukiwa na taarifa zisizothibitishwa kwamba, uchaguzi huo utafanyika mwaka 2021 kutokana na tishio la ugonjwa corona.

“Hatujazuiliwa kukutana, sisi tunaendelea kukutana na tunakutana katika mikutano ya kawaida, na uchaguzi tutafanya tu, wako wengine wanafikiri nitaahirisha, nani anataka kukaa kwenye maofisi muda wote huo?” amehoji Rais Magufuli.

Rais Magufuli amesema, kazi zitaendelea kufanyika ikiwemo vikao vya bunge vitaendelea.

“Hatujazuiliwa kukutana, leo nilikuwa nasoma gazeti moja linasema Madiwani wafanya kikao sijui alifikiri wamezuiliwa kukutana kwa sababu ya Corona? Sisi tunaendelea kukutana, hata nchi zilizoathirika, bado mabunge na mabaraza hayajafungwa,”amesema Rais Magufuli.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Bilioni 6.1 kumaliza tatizo la maji Katoro-Buseresere – Geita

Spread the loveMakamu mwenyekiti wa Umoja wa wanawake CCM, (UWT), Zainab Shomari...

Habari za SiasaTangulizi

Serikali kupokea ndege ya 14 ya ATCL, safari kuongezeka

Spread the love  SERIKALI ya Tanzania, kesho tarehe 3 Oktoba 2023, inatarajia...

Habari za Siasa

Serikali yawaangukia viongozi wa dini

Spread the loveSERIKALI imewaomba viongozi wa dini, waendelee kuelimisha wananchi kudumisha amani...

Habari za Siasa

Azzim Dewji aitaka Serikali iwanyooshe mafisadi

Spread the loveMFANYABIASHARA maarufu nchini, Azzim Dewji, ameitaka Serikali iwachukulie hatua wezi...

error: Content is protected !!