Friday , 3 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Dk. Vincent Mashinji azomewa kortini
Habari za Siasa

Dk. Vincent Mashinji azomewa kortini

Spread the love

DAKTARI Vincent Mashinji, aliyekuwa Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kabla ya kujiunga Chama cha Mapinduzi (CCM), amejikuta kwenye wakati mgumu baada ya kuzomewa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu. Anaripoti Hamis Mguta, Dar es Salaam…(endelea).

Leo tarehe 10 Machi 2020, Dk. Mashinji alikutana na zogo wakati anaingia katika chumba cha mahakama hiyo, kwa ajili ya kusikiliza hukumu ya Kesi ya Uchochezi Na.112/2018, inayomkabili na viongozi wakuu wa Chadema.

Alipokuwa anaingia katika chumba cha mahakama hiyo, Dk. Mashinji alianza kuzomewa na baadhi ya wafuasi wa Chadema.

Hata hivyo, alivyoingia Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa Chadema, shangwe ziliibuka huku watu wakiimba ‘Mwamba tuvushe’.

Muda huu watu wanaanza kuingia katika chumba cha mahakama kwa ajili ya kusubiri hukumu ya viongozi hao.

Washtakiwa katika kesi hiyo ni pamoja na Halima Mdee, Mwenyekiti Bawacha.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kumshtaki Rais Samia

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetishia kumfungulia kesi ya...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza uchaguzi mdogo Jimbo la Kwahani

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi, imetangaza uchaguzi mdogo...

AfyaHabari za Siasa

Dk. Biteko aagiza utoaji huduma saratani usiwe wa kibaguzi

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

error: Content is protected !!