Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Dk. Vincent Mashinji azomewa kortini
Habari za Siasa

Dk. Vincent Mashinji azomewa kortini

Spread the love

DAKTARI Vincent Mashinji, aliyekuwa Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kabla ya kujiunga Chama cha Mapinduzi (CCM), amejikuta kwenye wakati mgumu baada ya kuzomewa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu. Anaripoti Hamis Mguta, Dar es Salaam…(endelea).

Leo tarehe 10 Machi 2020, Dk. Mashinji alikutana na zogo wakati anaingia katika chumba cha mahakama hiyo, kwa ajili ya kusikiliza hukumu ya Kesi ya Uchochezi Na.112/2018, inayomkabili na viongozi wakuu wa Chadema.

Alipokuwa anaingia katika chumba cha mahakama hiyo, Dk. Mashinji alianza kuzomewa na baadhi ya wafuasi wa Chadema.

Hata hivyo, alivyoingia Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa Chadema, shangwe ziliibuka huku watu wakiimba ‘Mwamba tuvushe’.

Muda huu watu wanaanza kuingia katika chumba cha mahakama kwa ajili ya kusubiri hukumu ya viongozi hao.

Washtakiwa katika kesi hiyo ni pamoja na Halima Mdee, Mwenyekiti Bawacha.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!