Tuesday , 30 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Mtatiro aagiza AMCOS Ruvuma vichunguzwe
Habari Mchanganyiko

Mtatiro aagiza AMCOS Ruvuma vichunguzwe

Julius Mtatiro, Mkuu wa Wilaya ya Tunduru
Spread the love

JULIUS Mtatiro, Mkuu wa Wilaya ya Tunduru mkoani Ruvuma, ameagiza Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), kuchunguza Vyama vya Ushirika vya Mazao (AMCOS), juu ya matumizi mabaya ya fedha za mauzo ya zao la korosho. Anaripoti Mwandishi Wetu, Ruvuma … (endelea).

Mtatiro ametoa agizo hilo jana tarehe 20 Februari 2020, wakati akifungua mafunzo ya vyama hivyo na vyama vya akiba na mikopo, mkoani Ruvuma.

Kiongozi huyo wa wilaya ya Tunduru amedai kwmaba, kuna baadhi ya viongozi wa AMCOS wanatumia fedha za korosho kutoa rushwa, ili wapitishwe katika uchaguzi wa vyama hivyo, unaotarajia kufanyika hivi karibuni.

Mtatiro amedai kuwa, baada ya uchaguzi wa AMCOS kutangazwa, viongozi wa vyama hivyo wasio waadilifu, wameanza kupitisha fedha.

“Serikali iko makini, kwa uzoefu wangu nimeupata kwenye msimu huu wa korosho unanitosha kabisa kuanza kujua nini kinaendelea kwenye korosho. Umetangazwa uchaguzi watu wnaanza kupitisha hela kwenye AMCOS na nimeshawaambia TAKUKURU waanze kazi yao na tunawajua,” amedai Mtatiro na kuongeza:

“Ttunajua hela zinatoka wapi na katika uchaguzi watu ndio wanaanza kuweka hela kwenye AMCOS mimi sina maslahi kwenye korosho nitasimama upande wa wakulima viongozi na watendaji wanaotumia maadili kuhakikisha mazao haya yanaleta tija kwa wakulima.”

Mtatiro amewaonya vigogo wa AMCOS wanaoshiriki uchaguzi huo  kutofanya vitendo vya kuhujumu watu wengine wasishiriki uchaguzo huo.

“Zoezi la uchaguzi la mwaka huu ni makini sisi tunaratibu, tunajua wapi tutakukuta. Utakeleta choko choko sisi tutamshuhulikia, acheni watu wachukue fomu wao ambao hawataki kupumzika waache. Pangeni jichagueni peke yenu, pingeni wengine wasichukue fomu, kuna wengine wanasema nikitolewa kwenye AMCOS yangu hakutakalika, kusikalike? tuna njia nyingi tutakushughulikia,” ameonya Mtatiro.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

7 wafa Ulanga, mbunge alia kutelekezwa na mawaziri, Tanroad

Spread the loveWatoto saba wamepoteza maisha na zaidi ya kaya 70 kukosa...

Habari Mchanganyiko

Bil 12.4 zimetumika ujenzi wa miradi wilaya ya Momba

Spread the love MKUU wa wilaya ya Momba mkoani Songwe Kennan Kihongosi...

AfyaHabari Mchanganyiko

Songwe katika mikakati ya elimu ya lishe kudhibiti udumavu

Spread the love  SERIKALI mkoani Songwe imejipanga kuendelea kutoa elimu ya lishe...

Habari Mchanganyiko

NBC yapata tuzo ya mwezeshaji bora wa mikopo serikali Afrika

Spread the loveBenki ya NBC imepata tuzo ya Mwezeshaji Bora wa Pamoja...

error: Content is protected !!