Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Madaktari wapya; JPM atoa masharti
Habari za Siasa

Madaktari wapya; JPM atoa masharti

Spread the love

RAIS John Magufuli amemuagiza Kapteni Mstaafu , George Mkuchika,  Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi na Utawala Bora, kuajiri madaktari wapya 1,000. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Rais Magufuli ametoa agizo hilo leo tarehe 20 Februari 2020, wakati akihutubia katika maadhimisho ya siku ya madaktari Tanzania, iliyofanyika jijini Dar es Salaam.

Hata hivyo, ametoa masharti kwamba madaktari wanaotakiwa kuajiriwa, ni wale ambao waliokaa zaidi ya miaka mitano bila ajira. kwasasa, madaktari 2,700 hawana ajira nchini.

Kiongozi huyo wa nchi ameagiza madaktari hao watakapoajiriwa, wasambazwe nchi nzima hasa katika maeneo ya vijijini na pembezoni mwa mji.

“Nifahamu tuna madaktari 2,700 bado hawajaajiriwa nitaifanyia kazi, nafikiri tutaanza polepole hata tukaichukua 1000, tuanze na 1,000 mambo yakiwa mazuri tena tuendelea kuajiri. Sababu tuna hospitali vijijini wanahitaji madaktari, na hapa tunaajiri madaktari tu walioahangaika miaka 5. Na wasambazwe vizuri katika mikoa yote,” ameagiza Rais Magufuli.

Rais Magufuli ametoa agizo hilo baada ya Dk. Elisha Osati, Rais wa Chama cha Madaktari Tanzania (MAT), kumuomba atatue changamoto ya ukosefu wa ajira kwa madaktari, pamoja na kuboresha masilahi yao.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanamke Rwanda ataka kupambana tena na Kagame

Spread the loveKIONGOZI wa kihistoria wa upinzani nchini Rwanda, Victoire Ingabire Umuhoza,...

Habari za Siasa

Wizara ya Kilimo yapanga kutumia Sh. 1.2 trilioni 2024/25

Spread the loveWIZARA ya Kilimo, imepanga kutumia bajeti ya Sh. 1.2 trilioni...

Habari za SiasaTangulizi

Serikali yaanza msako wanaotoa mikopo kausha damu

Spread the loveSERIKALI imeanza kufuatilia watu, vikundi na taasisi zinazotoa kinyume cha...

Habari za Siasa

Spika Tulia aibana Serikali mafao ya wastaafu Jumuiya ya Afrika Mashariki

Spread the loveSPIKA wa Bunge, Dk. Tulia Ackson ameitaka Serikali kufanya tathimini...

error: Content is protected !!