Saturday , 9 December 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Wadhamini wataka Lissu akamatwe
Habari za SiasaTangulizi

Wadhamini wataka Lissu akamatwe

Spread the love

WADHAMINI wa Tundu Lissu, leo tarehe 20 Februari 2020, wameiomba Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, jiijini Dar es Salaam kutoa hati ya kumkamata mdaminiwa wao (Lissu). Anaripoti Faki Sosi, Dar es Salaam … (endelea).

Ibrahim Ahmed na Robart Katula, wameieleza mahakama kwamba, juhudi zao za kumfikisha mahakamani hapo Lissu, aliyekuwa Mbunge wa Singida Mashariki zimegonga mwamba, na sasa wanaiomba mahakama kuwasaidia.

Maombi ya wadhamini hao, yamefikishwa wakati shauri hilo lilipotajwa mbele ya Hakimu  Mkazi Mkuu, Thomas Simba.

Awali, wakili wa serikali mwandamizi Wankyo Simon, amedai upande wa mashtaka umepokea maombi kutoka kwa wadhamini wa mshtakiwa huyo, ya kuomba kumkamata ili waweze kujitoa kwenye udhamini huo.

Wankyo amedai, upande wa mashtaka umeridhia kusikilizwa maombi hayo, ambapo wameomba yasikilizwe kesho tarehe 21 Februari 2020.

Katula amedai kuwa, wameshindwa kumkamata na kumleta mshtakiwa huyo kwa nguvu zao, hivyo wanaomba kusikilizwa kwa maombi hayo.

Baada ya kusikiliza hoja hizo, Hakimu  Simba amehairisha shauri hilo kesho, ambapo pande zote zitakuja kuangalia taratibu za kisheria juu ya maombi hayo na kusisitiza kuwa, amri za kesi ya msingi bado zinaendelea kuwa na nguvu.

Mbali na Lissu, washtakiwa wengine kwenye kesi hiyo ni Simon Mkina, ni mhariri wa gazeti la MAWIO; Jabir Idrissa, mwandishi wa gazeti hilo na Ismail Mehbob, mfanyakazi wa kampuni ya uchapishaji ya magazeti ya Jamana. Wanakabiliwa na mashitaka matano katika mahakama hapo, likiwamo uchochezi.

Wote wanne, wanatuhumiwa kuandika, kuchapisha na kusambaza taarifa hizo kwenye gazeti la MAWIO la tarehe 14 Januari 2016, kinyume na Sheria ya Magazeti ya Mwaka 2002. Habari ambayo inadaiwa kuwa ya uchochezi, ilibeba kichwa cha maneno kisemacho: “Machafuko yaja Zanzibar.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Mbowe: Miaka 62 ya uhuru tujenge upya mioyo yetu

Spread the loveWAKATI Tanganyika ikiadhimisha miaka 62 tangu kupata uhuru, Mwenyekiti wa...

Habari za Siasa

Rais Samia asamehe wafungwa 2,244

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amewasamehe wafungwa 2,244, huku akiwabadilishia...

Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia ataka jamii inayohoji mafisadi

Spread the loveRAIS Samia Suluhu Hassan ametoa maagizo juu ya uboreshaji dira...

Habari za SiasaTangulizi

Kapinga: Kukatika kwa umeme siyo hujuma

Spread the loveNaibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga amesema Serikali ipo kazini...

error: Content is protected !!