Thursday , 2 May 2024
Habari za Siasa

Sumaye arudi CCM

Spread the love

FREDERICK Sumaye, Waziri Mkuu wa zamani amerejea katika Chama Cha Mapinduzi (CCM), leo tarehe 10 Februari 2020. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Sumaye ametangaza kurejea akiwa kwenye ofisi ndogo ya chama hicho Mtaa wa Lumumba, jijini Dar es Salaam ambapo amepokewa na Dk Bashiru Ally, katibu mkuu wa chama hicho.

Sumaye aliyehuduma kama Waziri Mkuu kwa miaka 10 katika serikali ya Rais wa Awamu ya Tatu, Benjamin Mkapa, ametangaza kurejea CCM kwenye kikao cha ndani cha chama hicho kilichokuwa kikiendelea leo.

Hatua ya Sumaye kuhamia CCM imetanguliwa na kujivua uanachama wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), zaidi ya miezi miwili iliyopita.

Alijivua uanachama Chadema kwa kile alichokiita ‘figisu’ kwenye uchaguzi wa Uenyekiti wa Kanda ya Pwani Chadema, ambapo licha ya kuwa mgombea pekee, lakini alipigiwa kura nyingi za hapana.

Tarehe 22 Agosti 2015, Sumaye alijiengua CCM na kuhamia Chadema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Spika Tulia aibana Serikali mafao ya wastaafu Jumuiya ya Afrika Mashariki

Spread the loveSPIKA wa Bunge, Dk. Tulia Ackson ameitaka Serikali kufanya tathimini...

Habari za Siasa

Serikali yawapa maagizo Ma-RC udhibiti magonjwa yasiyoambukiza

Spread the loveWAKUU wa mikoa nchini wametakiwa kuandaa utaratibu wa kuwawezesha wananchi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

error: Content is protected !!