Wednesday , 1 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Zitto ashtukia “wananitafuta wanifungulie kesi”
Habari za Siasa

Zitto ashtukia “wananitafuta wanifungulie kesi”

Spread the love

ZITTO Kabwe Kiongozi wa Chama cha ACT-Wazalendo ameeleza kuwa zipo njama zinazofanywa dhidi yake ili akamatwe na kushtakiwa kwa kesi ya utakashaji fedha kwa lengo la kumfanya akose kushiiriki uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2020, Anaripoti Mwandishi wetu, Kigoma … (endelea).

Akizungumza na wafuasi wa chama hicho mkoani Kigoma amesema kuwa anatafutwa kwa dhamira ya kutengezewa kesi ya utakatishaji fedha ambayo haina dhamana ila asishiriki uchaguzi Mkuu wa kumchagua Madiwani, Wabunge na Rais.

“Mimi najua wananitafuta sasa hivi wanitengezee kesi ya utakatishaji fedha ili waniweke ndani uchaguzi unikute niko ndani…” amesema Zitto.

Amesema kuwa njama za awali ni kumzuia asichukue fomu ya kugombea nafasi anayokusudia lakini wameona hawataweza wakaona wabadilishe namna.

“Wameamua ama wazuie nisichukue fomu au waniweke ndani, wameona bora waniweke ndani hivi sasa viongozi wetu, madiwani wetu wameitwa Takukuru leo, karibu viongo wetu wote wameitwa Takukuru.

“Kuna diwani mmoja wa Mwandiga alikuwa Mwenyekiti wa serikali ya kijiji zamani wakati ule ndio nimekuwa Mbunge  nikawa nataka nijenge nyumba nikaomba kiwanja kwenye Serikali ya kijiji, wakamuandikia barua kwamba tuletee maombi yote aliyofanya Zitto ya kuomba viwanja na ardhi eti wanachunguza taarifa zangu zote. Nimeweka wazi  na miaka yote naweka wazi hamna kitu kipya watakachokutana nacho…” amesema Zitto.

Amesema kuwa wanaweza kumtengenezea shauri hilo kwa kuwa tayari wamekusudia  “wanaweza kutengeza mashtaka yoyote na wala mkisikia msishangae kwa sababu hawana namna ya kushinda na sisi kwa hoja,” amesema Zitto.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

error: Content is protected !!