Thursday , 28 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Zitto alianzisha Kigoma, wenyeviti CCM ‘walia njaa’
Habari za SiasaTangulizi

Zitto alianzisha Kigoma, wenyeviti CCM ‘walia njaa’

Spread the love

WAJUMBE wa Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji, wamegoma kuwatambua wenyeviti wa serikali za mitaa waliopita bila kupingwa. Anaripoti Mwandishi Wetu, Kigoma … (endelea).

Wajumbe wa baraza hilo wameazimia wenyeviti hao wasilipwe posho, kwa madai kwamba sio viongozi halali, kwa kuwa hawakuchaguliwa na wananchi.

Azimio hilo limepitishwa kikao cha Baraza la Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji, lililokutana katika kikao chake cha kwanza kwa mwaka 2020.

Uamuzi huo umefikiwa baada ya Obadia Andrea Manwingi, Diwani wa Katubuka kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), kuhoji kwamba lini halmashauri hiyo itapeleka posho hizo kwa wenyeviti wa serikali za mitaa, vitongoji na vijiji.

Baada ya hoja hiyo, Zitto Kabwe, Mbunge wa Kigoma Mjini aliwataka wajumbe wa baraza hilo, kuweka azimio la kushinikiza halmashauri hiyo isitoe posho kwa wenyeviti, kwa madai kwamba fedha za walipa kodi haziwezi kutumiwa na viongozi wasio na ridhaa ya wananchi.

“Mheshimiwa Diwani, naomba usahau kuhusu malipo ya posho kwa wenyeviti hawa waliowekwa bila ridhaa ya wananchi, mpaka baraza hili linamaliza muda wake. Hatuwezi kutumia kodi za wananchi kuwalipa wenyeviti haramu, wasitegemee ushirikiano wowote na baraza hili ,” amesema Zitto.

“ACT Wazalendo inatoa wito kwa wananchi na vyama makini vya upinzani, vinavyoongoza halmashauri kutowatambua wenyeviti hawa haramu na kutowapa ushirikiano wowote kiutendaji.”

Kikao hicho kiliongozwa na Mstahiki Meya Hussein Ruhava. Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji ina Kata 19 Mitaa 68 na Madiwani 18 ACT Wazalendo, 7 CCM  na 1 CHADEMA.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanaye rais jela miaka miaka 6 kwa dawa za kulevya

Spread the loveMwanawe rais wa zamani wa Guinea-Bissau amehukumiwa kifungo cha miaka...

Habari za SiasaTangulizi

Mapya yaibuka wamasai waliohamishwa Ngorongoro kwenda Msomera

Spread the loveMAPYA yameibuka kuhusu zoezi la Serikali kuwahamisha kwa hiari wamasai...

Habari MchanganyikoTangulizi

Baba aomba msaada kuzika miili ya familia yake iliyofunga bila kula kuonana na Mungu

Spread the loveWAKATI Mamlaka nchini Kenya, ikiendelea kukabidhi miili ya watu waliofariki...

Habari za Siasa

Rais Samia ampongeza mpinzani aliyeshinda urais Senegal

Spread the loveRAIS wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan, amempongeza mwanasiasa wa...

error: Content is protected !!