Friday , 3 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa JPM azungumzia uchaguzi 2020, aonya wanaopanga kufanya fujo
Habari za Siasa

JPM azungumzia uchaguzi 2020, aonya wanaopanga kufanya fujo

Rais John Magufuli
Spread the love

RAIS John Magufuli amewataka Watanzania kujiandaa vyema, katika kushiriki Uchaguzi Mkuu  wa mwaka huu.Anaripoti Regina Mkonde…(endelea).

Rais Magufuli ametoa wito huo wakati akitoa salamu za kheri ya mwaka mpya kwa Watanzania, leo tarehe 11 Januari 2020, katika ziara yake Visiwani Zanzibar .

“Mwaka huu uwe wa amani na mafanikio, kama mjuavyo baadae mwaka huu nchi yetu inafanya uchaguzi mkuu, hivyo nawasihi wote tujiandae kushiriki uchaguzi huo vizuri. Na bila kusahau kumuomba Mungu aendelee kulilinda na kulisimamia taifa letu,” amesema Rais Magufuli.

Wakati huo huo, Rais Magufuli amewaonya watu wanaopanga kufanya fujo katika uchaguzi huo.

“Ukiona kuna amani ujue kuna watu hawalali, kwa sababu wale ambao wangependa nchi hii isiwe na amani wapo, na vibaraka hawaishi walikuwepo hata enzi za mitume. Hata Mungu aliumba malaika lakini wengine waligoma wakata wawe kama yeye akawafukuza wakawa mashetani.

Kwa hiyo vibaraka wataendelea kuwepo, saa nyingine mnaweza kufanya uchaguzi ukamaliza mwingine akasema nitaapishwa tu, msubiri nitakuja kuapishwa,” ameeleza Rais Magufuli

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kumshtaki Rais Samia

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetishia kumfungulia kesi ya...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza uchaguzi mdogo Jimbo la Kwahani

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi, imetangaza uchaguzi mdogo...

AfyaHabari za Siasa

Dk. Biteko aagiza utoaji huduma saratani usiwe wa kibaguzi

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

error: Content is protected !!