Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa JPM azungumzia uchaguzi 2020, aonya wanaopanga kufanya fujo
Habari za Siasa

JPM azungumzia uchaguzi 2020, aonya wanaopanga kufanya fujo

Rais John Magufuli
Spread the love

RAIS John Magufuli amewataka Watanzania kujiandaa vyema, katika kushiriki Uchaguzi Mkuu  wa mwaka huu.Anaripoti Regina Mkonde…(endelea).

Rais Magufuli ametoa wito huo wakati akitoa salamu za kheri ya mwaka mpya kwa Watanzania, leo tarehe 11 Januari 2020, katika ziara yake Visiwani Zanzibar .

“Mwaka huu uwe wa amani na mafanikio, kama mjuavyo baadae mwaka huu nchi yetu inafanya uchaguzi mkuu, hivyo nawasihi wote tujiandae kushiriki uchaguzi huo vizuri. Na bila kusahau kumuomba Mungu aendelee kulilinda na kulisimamia taifa letu,” amesema Rais Magufuli.

Wakati huo huo, Rais Magufuli amewaonya watu wanaopanga kufanya fujo katika uchaguzi huo.

“Ukiona kuna amani ujue kuna watu hawalali, kwa sababu wale ambao wangependa nchi hii isiwe na amani wapo, na vibaraka hawaishi walikuwepo hata enzi za mitume. Hata Mungu aliumba malaika lakini wengine waligoma wakata wawe kama yeye akawafukuza wakawa mashetani.

Kwa hiyo vibaraka wataendelea kuwepo, saa nyingine mnaweza kufanya uchaguzi ukamaliza mwingine akasema nitaapishwa tu, msubiri nitakuja kuapishwa,” ameeleza Rais Magufuli

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!