Wednesday , 8 May 2024
Home Kitengo Maisha Elimu ‘Wahadhiri walazimisha ngono vyuoni’
ElimuHabari Mchanganyiko

‘Wahadhiri walazimisha ngono vyuoni’

Dk. John Jingu, Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto
Spread the love

SERIKALI imetoa onyo kutokana na kushamiri kwa vitendo vya rushwa ya ngono katika vyuo vya elimu ya juu. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).

Dk. John Jingu, Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto amesema, zipo taarifa kwamba wahadhiri wengi wamekuwa wakitumia madaraka yao ‘kuwala’ wanachuo ili wawafaulishe.

Akizungumza kwenye ufunguzi wa kikao kilichowakutanisha wakuu wa vyuo vya elimu ya juu, kilicholenga mapambano dhidi ya ukatili wa kijinsia vyuo vya elimu ya juu tarehe 23 Desemba 2019, Dk. John Jingu amesema, wadhadhiri wamekuwa wakilazimisha wanafunzi kufanya nao ngono.

Amesema, imebainika kwamba si wanafunzi wote wanaopenda ama kujirahisisha kutenda vitendo hivyo, bali wahadhiri ndio wamekuwa wakitumia mwanya wa mamlaka yao kushawishi ili kukubaliwa.

Aemefafanua kwamba, hata wafanyakazi katika vyuo vya elimu ya juu, nao wamakumbwa na mkondo huo wa ukatili.

“Tunapaswa kukemea tabia hii. Tumeshuhudia vitendo vya namna hii kuwepo kwenye vyuo vyetu,” amesema Dk. Jingu.

Amewataka wakuu wa vyuo kuanzisha madawati ya jinsia katika vyuo vyao, ili kuondokana na vitendo vya kikatili na kujenga mazingira yaliyo salama katika vyuo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Rais Samia: Matumizi ya nishati safi sio anasa, ladha ipo

Spread the loveRAIS Samia Suluhu Hassan amesema matumizi ya nishati safi kwa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC, SILABU waungana kufikisha elimu ya fedha majumbani

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) imeingia makubaliano ya ushirikiano...

AfyaHabari MchanganyikoMakala & Uchambuzi

Kisukari cha mimba ni nini?

Spread the loveKisukari cha mimba ni aina ya kisukari kinachotokea kwa baadhi...

Habari Mchanganyiko

Mafunzo kwa bodaboda 395 yamkuna Meya Dodoma

Spread the loveNAIBU Meya wa Jiji la Dodoma, Asma Karama amepongeza mafunzo...

error: Content is protected !!