Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Zitto awapa tano Tundu Lissu, Mbowe
Habari za Siasa

Zitto awapa tano Tundu Lissu, Mbowe

Spread the love

ZITTO Kabwe Kiongozi wa Chama cha ACT-Wazalendo Zitto Kabwe amempongeza Freeman Mbowe, kwa kuchaguliwa tena kuwa Mwenyekiti  wa Chadema na Tundu Lissu kuwa Makamo Mwenyekiti wa Chama hicho. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).

Salamu hizo zilizotolewa na Ado Shaibu Katibu wa Itikadi Uenezi na Mawasiliano ya Umma wa ACT-Wazalendo, zimeleza kuwa Zitto na chama chake kinakipongeza Chadema kwa kufanikiwa kufanya mkutano mkuu, sambamba na kuchagua viongozi wao. 

Zitto amewahakikishia viongozi hao kuwa chama chake kitashikirikiana na Chadema na vyama vingine vyenye dhamira ya kuitetea na kupigania demokrasia.

Chadema kinataraji kuhitimisha kikao chake leo kwa kuteua nafasi ya Katibu Mkuu wa Chama hicho sambamba na manaibu makatibu wakuu Bara na Zanzibar.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

error: Content is protected !!