Wednesday , 1 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa JPM akerwa na mlundikano wa mahabusu, atoa agizo
Habari za Siasa

JPM akerwa na mlundikano wa mahabusu, atoa agizo

Rais John Magufuli
Spread the love

RAIS John Magufuli amesema ni aibu nchi kuwa na idadi kubwa ya mahabusu, kuliko wafungwa. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Kauli hiyo ameitoa leo tarehe 18 Desemba 2019, wakati akifungua jengo la Mahakama ya Wilaya ya Chato, mkoani Geita.

“Ni aibu kuwa na idadi kubwa ya mahabusu kuliko idadi ya wafungwa. Mnaweza mkaona changamoto tuliyonayo ya kupunguza mahabusu,” ameeleza Rais Magufuli.

Kufuatia changamoto hiyo, Rais Magufuli ameagiza vyombo vya dola kushirikiana na mahakama ili kuitatua changamoto hiyo.

Rais Magufuli amevitaka vyombo vinavyotoa haki kuimarisha mfumo wa utoaji haki ili kuharakisha uendeshaji wa mashtaka.

“Nitoe agizo kwa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), ofisi ya DPP, wakili mkuu wa serikali na polisi kushirikiana na mahakama ili kuimarisha mfumo wa haki na kuharakisha uendeshaji mashtaka nchini,” ameagiza Rais Magufuli.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

error: Content is protected !!