Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa JPM akerwa na mlundikano wa mahabusu, atoa agizo
Habari za Siasa

JPM akerwa na mlundikano wa mahabusu, atoa agizo

Rais John Magufuli
Spread the love

RAIS John Magufuli amesema ni aibu nchi kuwa na idadi kubwa ya mahabusu, kuliko wafungwa. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Kauli hiyo ameitoa leo tarehe 18 Desemba 2019, wakati akifungua jengo la Mahakama ya Wilaya ya Chato, mkoani Geita.

“Ni aibu kuwa na idadi kubwa ya mahabusu kuliko idadi ya wafungwa. Mnaweza mkaona changamoto tuliyonayo ya kupunguza mahabusu,” ameeleza Rais Magufuli.

Kufuatia changamoto hiyo, Rais Magufuli ameagiza vyombo vya dola kushirikiana na mahakama ili kuitatua changamoto hiyo.

Rais Magufuli amevitaka vyombo vinavyotoa haki kuimarisha mfumo wa utoaji haki ili kuharakisha uendeshaji wa mashtaka.

“Nitoe agizo kwa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), ofisi ya DPP, wakili mkuu wa serikali na polisi kushirikiana na mahakama ili kuimarisha mfumo wa haki na kuharakisha uendeshaji mashtaka nchini,” ameagiza Rais Magufuli.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!