Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa  Mchungaji Msigwa awavaa wanaoikosoa Chadema
Habari za Siasa

 Mchungaji Msigwa awavaa wanaoikosoa Chadema

Mch. Peter Msigwa
Spread the love

MCHUNGAJI Peter Msigwa, Mbunge wa Iringa Mjini amewashukia wafuasi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), wanao kikosoa chama hicho mitandaoni. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Kupitia ukurasa wake wa Twitter leo tarehe 16 Desemba 2019, Mchungaji Msigwa amewashauri wafuasi wa Chadema wenye maoni juu ya chama hicho, kupeleka ushauri wao kwenye vikao vya chama.

Mwenyekiti huyo wa Chadema Kanda ya Nyasa, amewashangaa wanachama hao wanaoshindwa kufikisha ushauri wao katika vikao vya chama, na badala yake wanapeleka madukuduku yao mitandaoni.

“Kuna vikao ambavyo vinaanzia kwenye msingi kwa sisi Chadema, mpaka taifa. Sasa wewe kama ni Mwana Chedema, kama una ushauri anzia huko.

Lakini wengi hawataki kuhudhuria huko , ila kwenye mitandao ndio mafundi wa kukosoa. Chama lazima kiwe na nidhamu, Chama ni vikao, lazima tuheshimu,” ameandika Mchungaji Msigwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

error: Content is protected !!