Friday , 19 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa  Mchungaji Msigwa awavaa wanaoikosoa Chadema
Habari za Siasa

 Mchungaji Msigwa awavaa wanaoikosoa Chadema

Mch. Peter Msigwa
Spread the love

MCHUNGAJI Peter Msigwa, Mbunge wa Iringa Mjini amewashukia wafuasi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), wanao kikosoa chama hicho mitandaoni. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Kupitia ukurasa wake wa Twitter leo tarehe 16 Desemba 2019, Mchungaji Msigwa amewashauri wafuasi wa Chadema wenye maoni juu ya chama hicho, kupeleka ushauri wao kwenye vikao vya chama.

Mwenyekiti huyo wa Chadema Kanda ya Nyasa, amewashangaa wanachama hao wanaoshindwa kufikisha ushauri wao katika vikao vya chama, na badala yake wanapeleka madukuduku yao mitandaoni.

“Kuna vikao ambavyo vinaanzia kwenye msingi kwa sisi Chadema, mpaka taifa. Sasa wewe kama ni Mwana Chedema, kama una ushauri anzia huko.

Lakini wengi hawataki kuhudhuria huko , ila kwenye mitandao ndio mafundi wa kukosoa. Chama lazima kiwe na nidhamu, Chama ni vikao, lazima tuheshimu,” ameandika Mchungaji Msigwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Tanzania, Uturuki zanuia kukuza biashara, uwekezaji

Spread the loveSERIKALI za Tanzania na Uturuki zimekubaliana kuendeleza dhamira ya kuimarisha...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza ajira watendaji daftari wapiga kura

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), imetangaza nafasi...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema yatangaza ruti awamu ya pili maandamano

Spread the love  CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimesema awamu ya...

Habari za Siasa

CCM yamkana mwenyekiti UVCCM aliyetaka wapinzani wapotezwe

Spread the love  CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimejitenga na kauli ya mwenyekiti...

error: Content is protected !!