Tuesday , 5 December 2023
Home Habari Mchanganyiko Wizara ya Elimu yaingilia kati ukata wa mikopo UDSM
Habari Mchanganyiko

Wizara ya Elimu yaingilia kati ukata wa mikopo UDSM

Bodi ya Mikopo Elimu ya Juu
Spread the love

WIZARA ya Elimu imeagiza Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HELSB),  kukutana na Uongozi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), ili kupata suluhu ya changamoto ya mikopo ya wanafunzi wa chuo hicho. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Agizo hilo limetolewa leo tarehe 16 Disemba 2019 na wizara hiyo, kupitia ukurasa wake wa Twitter, siku moja baada ya Uongozi wa Serikali ya Wanafunzi wa UDSM (DARUSO) kutoa saa 72 kwa HELSB, kutatua changamoto hiyo.

Wizara hiyo imeagiza HESLB na uongozi wa chuo hicho, kukutana na DARUSO leo, ili kutatua changamoto hizo.

Aidha, Wizara hiyo imewasihi wanafunzi wa chuo hicho kuwa watulivu na kuendelea na masomo yao, wakati changamoto zao zikishughulikiwa.

Jana tarehe 15 Disemba 2019, DARUSO ilitoa saa 72 kwa HESLB kutoa mikopo kwa wanafunzi, kurudisha fedha za mikopo za wanafunzi, ilizokata. Pamoja na kuwapangia mikopo wanafunzi wa mwaka wa kwanza, ambao rufaa zao zilitupingwa, huku wakiwa ni wahitaji wa mikopo hiyo.

Hatua hiyo imekuja baada ya Serikali hiyo kulalamika kwamba, kumekuwa na changamoto ya wanafunzi wanaondelea na masomo kutopewa mikopo, na wengine kukatwa fedha zao za mikopo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

RPC Songwe awafunda trafki kuzingatia uadilifu

Spread the loveASKARI wa kikosi cha usalama barabarani mkoani Songwe wametakiwa kuendelea...

Habari Mchanganyiko

Mchimba madini jela maisha kwa kubaka, alihonga Sh 500

Spread the loveMahakama ya wilaya ya Songwe imemtia hatiani na kumhukumu kifungo...

Habari Mchanganyiko

Mlima wa Moto wazindua kongamano la SHILO kumuenzi Rwakatare

Spread the loveKANISA la Mlima wa Moto Mikocheni jijini Dar es Salaam,...

Habari MchanganyikoTangulizi

20 wafariki dunia kwa mafuriko Manyara

Spread the loveMVUA za vuli zinazoendelea kunyesha maeneo mbalimbali nchini zimeleta madhara...

error: Content is protected !!