Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais anapotoshwa – LHRC
Habari za Siasa

Rais anapotoshwa – LHRC

Rais John Magufuli
Spread the love

ANNA Henga, Mkurugenzi wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), amesema baadhi ya wasaidizi wa Rais John Magufuli, wanampotosha kwa maslahi yao ya kisiasa. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Henga ametoa kauli hiyo tarehe 13 Desemba 2019, wakati alipozungumza na MwanaHALISI ONLINE, kuhusu tuhuma zilizotolewa na Rais Magufuli, kwamba kuna Asasi za Kiraia (AZAKI) na Mashirika Yasiyo ya Kiserikali (NGO’s), zinatumiwa na watu wasioitakia mema nchi.

Akizungumzia tuhuma hizo kwa ufupi, Henga amesema Rais Magufuli anapotoshwa na baadhi ya wasaidizi wake, kuhusu suala hilo.

“Baadhi ya wasaidizi wa Rais wanamuongoza vibaya kwa masilahi yao ya kisiasa,” amesema Henga.

Wakati akifungua semina ya wajumbe wa Halmshauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi (CCM), jijini Mwanza, aliekeza tuhuma kwa AZAKI na NGO’S, watu wasioitakia mema Tanzania, watatumia asasi hizo, kujifanya wanafundisha Demokrasia na haki za binadamu.

Wakati wao wanavunja misingi hiyo, kwa kujenga mifumo ya kinyonyaji, kuchochea machafuko na kuingilia uhuru wa mataifa mengine.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

error: Content is protected !!