Wednesday , 6 December 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Rais anapotoshwa – LHRC
Habari za Siasa

Rais anapotoshwa – LHRC

Rais John Magufuli
Spread the love

ANNA Henga, Mkurugenzi wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), amesema baadhi ya wasaidizi wa Rais John Magufuli, wanampotosha kwa maslahi yao ya kisiasa. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Henga ametoa kauli hiyo tarehe 13 Desemba 2019, wakati alipozungumza na MwanaHALISI ONLINE, kuhusu tuhuma zilizotolewa na Rais Magufuli, kwamba kuna Asasi za Kiraia (AZAKI) na Mashirika Yasiyo ya Kiserikali (NGO’s), zinatumiwa na watu wasioitakia mema nchi.

Akizungumzia tuhuma hizo kwa ufupi, Henga amesema Rais Magufuli anapotoshwa na baadhi ya wasaidizi wake, kuhusu suala hilo.

“Baadhi ya wasaidizi wa Rais wanamuongoza vibaya kwa masilahi yao ya kisiasa,” amesema Henga.

Wakati akifungua semina ya wajumbe wa Halmshauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi (CCM), jijini Mwanza, aliekeza tuhuma kwa AZAKI na NGO’S, watu wasioitakia mema Tanzania, watatumia asasi hizo, kujifanya wanafundisha Demokrasia na haki za binadamu.

Wakati wao wanavunja misingi hiyo, kwa kujenga mifumo ya kinyonyaji, kuchochea machafuko na kuingilia uhuru wa mataifa mengine.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Bashungwa: Katesh kutafanyiwa usafi wa hali ya juu

Spread the loveWAZIRI wa Ujenzi, Innocent Bashungwa amesema kazi ya kuondoa tope...

AfyaHabari za Siasa

RAS Songwe: Tumepigwa… mkurugenzi nakupa siku 21

Spread the loveKATIBU tawala mkoani Songwe, Happines Seneda ametoa siku 21 kwa...

Habari za Siasa

Dk. Biteko: Viongozi tuache alama nzuri katika utendaji wetu

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

Habari za SiasaTangulizi

Chanzo maporomoko yaliyoua 65 Hanang, chatajwa

Spread the loveSERIKALI imesema kumeguka kwa sehemu ya Mlima Hanang ambao ilikuwa...

error: Content is protected !!