Friday , 19 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais anapotoshwa – LHRC
Habari za Siasa

Rais anapotoshwa – LHRC

Rais John Magufuli
Spread the love

ANNA Henga, Mkurugenzi wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), amesema baadhi ya wasaidizi wa Rais John Magufuli, wanampotosha kwa maslahi yao ya kisiasa. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Henga ametoa kauli hiyo tarehe 13 Desemba 2019, wakati alipozungumza na MwanaHALISI ONLINE, kuhusu tuhuma zilizotolewa na Rais Magufuli, kwamba kuna Asasi za Kiraia (AZAKI) na Mashirika Yasiyo ya Kiserikali (NGO’s), zinatumiwa na watu wasioitakia mema nchi.

Akizungumzia tuhuma hizo kwa ufupi, Henga amesema Rais Magufuli anapotoshwa na baadhi ya wasaidizi wake, kuhusu suala hilo.

“Baadhi ya wasaidizi wa Rais wanamuongoza vibaya kwa masilahi yao ya kisiasa,” amesema Henga.

Wakati akifungua semina ya wajumbe wa Halmshauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi (CCM), jijini Mwanza, aliekeza tuhuma kwa AZAKI na NGO’S, watu wasioitakia mema Tanzania, watatumia asasi hizo, kujifanya wanafundisha Demokrasia na haki za binadamu.

Wakati wao wanavunja misingi hiyo, kwa kujenga mifumo ya kinyonyaji, kuchochea machafuko na kuingilia uhuru wa mataifa mengine.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Tanzania, Uturuki zanuia kukuza biashara, uwekezaji

Spread the loveSERIKALI za Tanzania na Uturuki zimekubaliana kuendeleza dhamira ya kuimarisha...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza ajira watendaji daftari wapiga kura

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), imetangaza nafasi...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema yatangaza ruti awamu ya pili maandamano

Spread the love  CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimesema awamu ya...

Habari za Siasa

CCM yamkana mwenyekiti UVCCM aliyetaka wapinzani wapotezwe

Spread the love  CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimejitenga na kauli ya mwenyekiti...

error: Content is protected !!