Sunday , 28 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa JPM: Ndege iliyoshikwa Canada, inakuja
Habari za SiasaTangulizi

JPM: Ndege iliyoshikwa Canada, inakuja

Moja ya ndege za Bombadier inayomilikiwa na Tanzania
Spread the love

RAIS John Magufuli amesema, ndege ya Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) Bombardier Q400, iliyoshikiliwa nchini Canada, imeachwa. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Akishiriki kwenye Semina ya Wajumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCMTaifa, Rais Magufuli amesema, ikianza safari ya kurejea nchini, mamlaka itatangaza na itapokelewa jijini Mwanza.

“Kwa taarifa tu, Ndege yetu iliyokuwa imeshikiliwa Canada imeachiwa, mtatangaziwa siku ya kuipokea na itapokelewa hapa Mwanza,” Rais Magufuli ambaye ni Mwenyekiti CCM Taifa, ametoa kauli hiyo leo tarehe 12 Desemba 2019.

Tarehe 23 Novemba 2019, mamlaka nchini Canada zilikamata ndege hiyo ilizuiwa kwa amri ya mahakama. Ilikuwa mara ya pili kwa ndege ya Tanzania kuzuiliwa nchini Canada.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba Kabudi alieleza, sababu ya kukamatwa kwa ndege hiyo, ni kesi iliyofunguliwa na mkulima mstaafu raia wa Namibia, Hermanus Steyn.

Steyn pia alifungua kesi nchini Afrika Kusini Agust iliyosababisha ndege aina ya Air Bus 220-300 izuiliwe.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Biteko aipongeza GGML kudhibiti vifo, majeruhi mahali pa kazi

Spread the loveNAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

Habari za Siasa

Askofu Shoo awataka ACT kupigania maslahi ya Taifa, wasikubali kuhongwa

Spread the loveALIYEKUWA Askofu Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri, Askofu...

Habari za Siasa

Biteko aagiza waajiri kudhibiti vifo mahali pa kazi

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde aibana kampuni kutimiza masharti ya mkataba

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameitaka Kampuni ya Xin Tai...

error: Content is protected !!