Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa JPM: Ndege iliyoshikwa Canada, inakuja
Habari za SiasaTangulizi

JPM: Ndege iliyoshikwa Canada, inakuja

Moja ya ndege za Bombadier inayomilikiwa na Tanzania
Spread the love

RAIS John Magufuli amesema, ndege ya Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) Bombardier Q400, iliyoshikiliwa nchini Canada, imeachwa. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Akishiriki kwenye Semina ya Wajumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCMTaifa, Rais Magufuli amesema, ikianza safari ya kurejea nchini, mamlaka itatangaza na itapokelewa jijini Mwanza.

“Kwa taarifa tu, Ndege yetu iliyokuwa imeshikiliwa Canada imeachiwa, mtatangaziwa siku ya kuipokea na itapokelewa hapa Mwanza,” Rais Magufuli ambaye ni Mwenyekiti CCM Taifa, ametoa kauli hiyo leo tarehe 12 Desemba 2019.

Tarehe 23 Novemba 2019, mamlaka nchini Canada zilikamata ndege hiyo ilizuiwa kwa amri ya mahakama. Ilikuwa mara ya pili kwa ndege ya Tanzania kuzuiliwa nchini Canada.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba Kabudi alieleza, sababu ya kukamatwa kwa ndege hiyo, ni kesi iliyofunguliwa na mkulima mstaafu raia wa Namibia, Hermanus Steyn.

Steyn pia alifungua kesi nchini Afrika Kusini Agust iliyosababisha ndege aina ya Air Bus 220-300 izuiliwe.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!