Tuesday , 30 April 2024
Home Kitengo Michezo Dewji afikia kikomo cha uvumilivu Simba
Michezo

Dewji afikia kikomo cha uvumilivu Simba

Mohammed Dewji 'MO'
Spread the love

MOHAMMED Dewji ‘Mo’ Mwekezaji wa klabu ya Simba, ameweka wazi kuwa klabu hiyo haitamvumilia mchezaji yeyote atakayeihujumu timu hiyo. Anaripoti Faki Sosi …(endelea).

Hayo ameyeweka wazi leo tarehe 8 Desemba 2019, kupitia ukurasa wake wa mtandao wa Twitter, amesema kuwa uongozi wa klabu hiyo unawalipa wachezaji hao hivyo nao wanatakiwa kuwajibika.

“Sisi tunawalipa vizuri mno, na wao wana wajibu wa kutulipa matokeo na furaha. Na ili furaha iwepo, lazima nidhamu isimamiwe kikamilifu, na katika hili hatutanii. Hatutajali ukubwa wa jina la mchezaji yoyote.” amesema ‘Mo’

Amesema kuwa matokeo mabaya kwa klabu hiyo itakuwa ndio mwisho wa uvumilivu wake.

“Simba lazima tuamue kuteseka na moja katika mambo haya mawili: (1) tuzoee uchungu na maumivu ya nidhamu au (2) maumivu ya matokeo mabaya. Kama mpenzi wa Simba, siwezi kujitoa wala kuvumilia matokeo mabaya kwa sababu ya mapungufu ya nidhamu.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Usiku wa Ulaya umerejea kibabe kabisa

Spread the love  LIGI ya Mabingwa barani Ulaya imerejea tena na awamu...

Michezo

Beti na Meridianbet mechi za leo

Spread the love IKIWA leo hii ni Jumapili tulivu kabisa, Meridianbet wanamkwambia...

Michezo

Jumamosi ya leo ni ya pesa tu kutoka Meridianbet

Spread the love  IKIWA leo hii ni Jumamosi nyingine na tulivu kabisa,...

Michezo

EPL, Ligue 1 na Coppa Italia kinawaka leo

Spread the love  LEO ligi kadhaa zitaendelea nchini barani ulaya ikiwemo ligi...

error: Content is protected !!