Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Passport ya Bulaya yaahirisha kesi
Habari za SiasaTangulizi

Passport ya Bulaya yaahirisha kesi

Spread the love

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es salaam, imeahirisha kusikiliza kesi inayowakabili viongozi waandamizi wa Chadema, kutokana na upande wa mashtaka kumtaka mshtakiwa wa tisa, Ester Bulaya, Mbunge wa Bunda Mjini, kuwasilisha mahakamani hapo hati ya kusafiria ili kuendelea kumhoji juu ya ushahidi wake. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).

Katika kesi hiyo namba 112 la mwaka 2018, Bulaya anashtakiwa pamoja na viongozi wanane wa chama hicho akiwemo, Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa Chadema-Taifa, Vicent Mashinji, Katibu Mkuu Chadema-Taifa, John Mnyika, Naibu Katibu Mkuu Chadema-Bara na Salum Mwalimu, Naibu Katibu Mkuu Chadema-Zanzibar.

Wengine ni Halima Mdee, Mbunge wa Kawe, John Heche, Mbunge wa Tarime Vijijini, Mch. Peter Msigwa, Mbunge wa Iringa Mjini na Ester Matiko, Mbunge wa Tarime Mjini.

Leo tarehe 6 Desemba 2019, Bulaya akiohojiwa na Wakili wa Serikali Mwandamizi, Wankyo Simon ameeleza kuwa tarehe 17 Februari, 2019, alimsindikiza Mdee kwenye hospitali ya St. Parrot nchini Afrika Kusini, kwa ajili ya matibabu.

Bulaya ameulizwa aina gani ya hati ya kusafiria aliyoitumia wakati alipomsindikiza hospitali Mdee amejibu kuwa ni hati ya kawaida.

Wankyo amemuuliza Bulaya iwapo upande wa mashtaka ukiitaka kuiona hati yake kusafiria amejibu kuwa siku yoyote kesi hiyo ikitaja ataiwasilisha.

Wakili wa Serikali Mkuu, Faraja Nchimbi ameiomba mahakama hiyo kuhairisha shauri hilo ili Bulaya akiwasilisha hati ya kusafiria ndipo wataendelea kumhoji.

Hakimu Simba ameahirisha shauri hilo mpaka tarehe 19 na 20 Desemba mwaka huu.

Washtakiwa wote wanatuhumiwa kwa makosa ya kutoa maneno ya uchochezi, kufanya kusanyiko lisilohalali na kufanya maandamano kinyume cha sheria yaliyodaiwa kusababisha kifo cha mwanafunzi wa Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT), Akwelina Akwelin.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

error: Content is protected !!