Thursday , 2 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Bombadier iliyokamatwa Canada, kuwasili nchini
Habari Mchanganyiko

Bombadier iliyokamatwa Canada, kuwasili nchini

Moja ya ndege za Bombadier inayomilikiwa na Tanzania
Spread the love

NDEGE iliyoshikiliwa nchini Canada kutokana na amri ya mahakama kufuatia kesi ya madai iliyofunguliwa na Hermanus Steyn, inataraji kuwasili Tanzania wakati wowote. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Taarifa hiyo imetolewa jana tarehe 28 Novemba 2019 na Injinia Isack Kamwelwe, Waziri wa Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi.

Kamwelwe ameeleza kuwa, mazungumzo kuhusu suala hilo yamekamilika, na kuwa, ndege hiyo aina ya Bombadier Q 400, itawasili wakati wowote, ingawa hakutaja siku.

Aidha, Kamwelwe amewataka Watanzania kuwa watulivu katika kipindi hiki ambacho juhudi za kuikomboa ndege hiyo zikiendelea.

Ndege hiyo mali ya serikali kwa ajili ya matumizi ya Kampuni ya Ndege ya Taifa (ATCL) imeshikiliwa nchini Canada, baada ya Steyn kufungua kesi katika mahakama ya nchi hiyo, akidai fidia ya mali zake zilizotaifishwa na serikali ya Tanzania mwaka 1980.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

NEMC yatoa elimu matumizi sahihi ya zebaki kwa wachimbaji

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC)...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Oryx gesi yagawa mitungi, majiko 100 kwa waandishi wa habari Dar

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gesi Tanzania imegawa mitungi 100 ya gesi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

error: Content is protected !!