Thursday , 28 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Lissu ‘ainusa’ Tanzania
Habari za Siasa

Lissu ‘ainusa’ Tanzania

Tundu Lissu, Makamu Mwenyekiti wa Chadema
Spread the love

TUNDU Lissu, aliyekuwa Mbunge wa Singida Mashariki yupo nchini Kenya, akisubiri ‘amri’ ya kuingia nchini endapo atahakikishiwa usalama wake. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Akizungumza na kituo cha Televisheni cha KTN nchini Kenya jana tarehe 28 Novemba 2019, Lissu amesema amepona lakini hali ya usalama wake bado si shwari.

“Bado kuna vitisho vya aina hii, lazima watu wenye busara wakae na kuangalia namna nzuri ya kufanya ili niweze kurudi nyumbani,” amesema Lissu.

Amemweleza mwandishi wa kituo hicho, kwamba kuna watu ambao wasingependa kuona akirudi na siku moja baadaye anapigwa risasi tena.

Lissu amesema “nafikiri hakuna mtu anayetaka kuona narudi nyumbani na keshokutwa ninapigwa risasi tena.”

Hata hivyo amesema, bado jitihada zinafanywa na ndani na nje ya nchi ili kuhakikisha ataporejea kunakuwa na usalama wa kutosha.

Amesisitiza, hataki kuishi nje ya Tanzania kwa kuwa, alikwenda kwa ajili ya matibabu na sasa matibabu hayo yamekwisha

“Mimi sitaki kabisa kuishi uhamishoni. Nilienda kwenye matibabu nimeshatibiwa nasubiri niambiwe usalama wangu utakuwaje katika mazingira halisi,” amesema.

Lissu alishambiliwa kwa risasi tarehe 7 Septemba 2017, akiwa nyumbani kwake eneo la ‘Area D’ jijini Dodoma na kupatiwa matibabu katika hospitali ya rufaa mkoa huo.

Baadaye alihamishiwa Nairobi nchini Kenya ambapo tarehe 6 Januari 2018 alipelekwa nchini Ubelgiji kwa matibabu zaidi ambapo yupo mpaka sasa.

Shambulizi dhidi ya Lissu, lilitokea muda mfupi baada ya kutoka kwenye mkutano wa Bunge wa asubuhi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!