Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Lissu ‘ainusa’ Tanzania
Habari za Siasa

Lissu ‘ainusa’ Tanzania

Tundu Lissu, Makamu Mwenyekiti wa Chadema
Spread the love

TUNDU Lissu, aliyekuwa Mbunge wa Singida Mashariki yupo nchini Kenya, akisubiri ‘amri’ ya kuingia nchini endapo atahakikishiwa usalama wake. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Akizungumza na kituo cha Televisheni cha KTN nchini Kenya jana tarehe 28 Novemba 2019, Lissu amesema amepona lakini hali ya usalama wake bado si shwari.

“Bado kuna vitisho vya aina hii, lazima watu wenye busara wakae na kuangalia namna nzuri ya kufanya ili niweze kurudi nyumbani,” amesema Lissu.

Amemweleza mwandishi wa kituo hicho, kwamba kuna watu ambao wasingependa kuona akirudi na siku moja baadaye anapigwa risasi tena.

Lissu amesema “nafikiri hakuna mtu anayetaka kuona narudi nyumbani na keshokutwa ninapigwa risasi tena.”

Hata hivyo amesema, bado jitihada zinafanywa na ndani na nje ya nchi ili kuhakikisha ataporejea kunakuwa na usalama wa kutosha.

Amesisitiza, hataki kuishi nje ya Tanzania kwa kuwa, alikwenda kwa ajili ya matibabu na sasa matibabu hayo yamekwisha

“Mimi sitaki kabisa kuishi uhamishoni. Nilienda kwenye matibabu nimeshatibiwa nasubiri niambiwe usalama wangu utakuwaje katika mazingira halisi,” amesema.

Lissu alishambiliwa kwa risasi tarehe 7 Septemba 2017, akiwa nyumbani kwake eneo la ‘Area D’ jijini Dodoma na kupatiwa matibabu katika hospitali ya rufaa mkoa huo.

Baadaye alihamishiwa Nairobi nchini Kenya ambapo tarehe 6 Januari 2018 alipelekwa nchini Ubelgiji kwa matibabu zaidi ambapo yupo mpaka sasa.

Shambulizi dhidi ya Lissu, lilitokea muda mfupi baada ya kutoka kwenye mkutano wa Bunge wa asubuhi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Sauti ya Watanzania waeleza sababu za kuiunga mkono Chadema

Spread the love  KIKUNDI kinachojipambanua katika kupigania rasilimali na uhuru wa nchi,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

error: Content is protected !!