Thursday , 2 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Tapeli wa fedha kupitia ATM akamatwa
Habari Mchanganyiko

Tapeli wa fedha kupitia ATM akamatwa

SACP Lazaro Mambosasa, Kamanda wa Polisi wa Kanda Dar es Salaam
Spread the love

JESHI la Polisi, Kanda Maalum ya Dar es Salaam linamshikilia Halima Juma (23), Mkazi wa Chalinze kwa tuhuma za wizi wa fedha kupitia mashine za kutolea fedha (ATM). Anaripoti Hamis Mguta …  (endelea).

SACP Lazaro Mambosasa, Kamanda wa Polisi wa Kanda hiyo amesema, Halima anashikiliwa mara baada ya kutiliwa shaka.

Amesema, tarehe 19 Novemba 2019 katika benki ya CRDB, tawi la Mbagala akiwa katika ATM, alitiliwa shaka baada ya kuingia kwenye chumba cha ATM ya benki hiyo akijifanya kuwasaidia wazee na wastaafu wasiojua kutumia mashine hizo.

“Lengo lake ni kuchukua namba za siri za wastaafu na wazee hao, kisha kuwabadilishia ATM kadi zao na baadaye kuwaibia fedha kwenye akaunti zao kwa kutumia kadi halisi za wahusika,” amesema na kuongeza;

“Mtuhumiwa huyo alikamatwa na askari wanaolinda Benki hiyo, na alipopekuliwa alikutwa na kadi 23 za watu mbalimbali za benki tofauti, zikiwa katika pochi yake huku akiwa amezificha katika sehemu zake za ukeni.”

Kamanda Mambosasa amewataka wastaafu kuwa makini na wizi wa aina hiyo, na kuhakikisha wanaongozana na watu wanaowaamini kwa msaada wa kutoa pesa katika mashine hizo.

Kadi alizokutwa nazo ni CRDB 07, NMB  06, NBC 02, AMANA  02, Pasta Benk 02, ACB  01, STANIBIC  01, DTB  01 na EQUITY 01.

Amesema, mtuhumiwa anaendelea kuhojiwa na atafikishwa mahakamani hivi karibuni.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

NEMC yatoa elimu matumizi sahihi ya zebaki kwa wachimbaji

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC)...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Oryx gesi yagawa mitungi, majiko 100 kwa waandishi wa habari Dar

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gesi Tanzania imegawa mitungi 100 ya gesi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

error: Content is protected !!