Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa JPM amnanga RC aliyemtumbua
Habari za Siasa

JPM amnanga RC aliyemtumbua

Spread the love

RAIS John Magufuli amemnanga Dk. Steven Kebwe, aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Morogoro kwa madai ya ‘kujimegea.’ Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Amesema, alijisahau na baadhi ya miradi kwenye halmashauri ilikuwa yake, akieleza mfano kwamba alipeleka mbao za hoyo kwenye halmashauri moja mkoani humo.

Rais Magufuli ametoa kauli hiyo leo tarehe 20 Novemba 2019, mkoani Morogoro wakati akizungumza na wakazi wa mkoa huo.

Amemsifu mkuu wa mkoa huo wa sasa, ambaye alikuwa Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mkoa wa Arusha, Loota Sanare kwamba ameanza kazi vizuri.

“…umeanza vizuri, endelea kuchaa kazi. Umeanza vizuri endelea kushughuikia kero zote, nataka niseme wazi, mkuu wa mkoa aliyekuwepo alijisahau.

“Baadhi ya miradi mingine hata kwenye halmashauri ilikuwa yake, kuna halmashauri ali – supply mbao za ovyo, ninayajua yote,” amesema Rais Magufuli.

Akimsife Sanare, Rais Magufuli amesema, ameanza kushughulikia kero za wananchi wa Morogoro na kumwagiza kuendelea kukabili matatizo ya mkoa huo.

“Shughulikia kero za wananchi hawa, shughulikia migogoro ya wafugaji na wakulima, nayo iishe sababu saa nyingine wakati wa kilimo, wakulima wanalima huku wafugaji wanakwenda kulisha mazao.

“Wanapeleka ng’ombe kwenye mazao, nimekuleta uwadhibiti hapa, ili Morogoro iwe na amani, wananchi waishi kwa amani,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

error: Content is protected !!