Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa JPM amnanga RC aliyemtumbua
Habari za Siasa

JPM amnanga RC aliyemtumbua

Spread the love

RAIS John Magufuli amemnanga Dk. Steven Kebwe, aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Morogoro kwa madai ya ‘kujimegea.’ Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Amesema, alijisahau na baadhi ya miradi kwenye halmashauri ilikuwa yake, akieleza mfano kwamba alipeleka mbao za hoyo kwenye halmashauri moja mkoani humo.

Rais Magufuli ametoa kauli hiyo leo tarehe 20 Novemba 2019, mkoani Morogoro wakati akizungumza na wakazi wa mkoa huo.

Amemsifu mkuu wa mkoa huo wa sasa, ambaye alikuwa Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mkoa wa Arusha, Loota Sanare kwamba ameanza kazi vizuri.

“…umeanza vizuri, endelea kuchaa kazi. Umeanza vizuri endelea kushughuikia kero zote, nataka niseme wazi, mkuu wa mkoa aliyekuwepo alijisahau.

“Baadhi ya miradi mingine hata kwenye halmashauri ilikuwa yake, kuna halmashauri ali – supply mbao za ovyo, ninayajua yote,” amesema Rais Magufuli.

Akimsife Sanare, Rais Magufuli amesema, ameanza kushughulikia kero za wananchi wa Morogoro na kumwagiza kuendelea kukabili matatizo ya mkoa huo.

“Shughulikia kero za wananchi hawa, shughulikia migogoro ya wafugaji na wakulima, nayo iishe sababu saa nyingine wakati wa kilimo, wakulima wanalima huku wafugaji wanakwenda kulisha mazao.

“Wanapeleka ng’ombe kwenye mazao, nimekuleta uwadhibiti hapa, ili Morogoro iwe na amani, wananchi waishi kwa amani,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!