Thursday , 2 May 2024
Home Kitengo Michezo Zembwela aitosa East Afrika Radio, atua Wasafi
Michezo

Zembwela aitosa East Afrika Radio, atua Wasafi

Spread the love

ALIYEKUWA mtangazaji wa East Africa Radio na East Africa Television kwa zaidi ya miaka sita, Hillary Daudi ‘Zembwela’ amekihama rasmi kituo hicho na kujiunga na kituo cha Wasafi Media kinachomiliki Wasafi FM na Wasafi TV. Anaripoti Kelvin Mwaipungu … (endelea).

Zembwela ambaye alikua akitangaza kipindi cha Supamix cha East Africa Radio pamoja na kipindi cha Uswazi cha EATV, ameanza kuonekana na kusikika leo kupitia Wasafi FM na Wasafi TV katika kipindi cha uchambuzi wa magazeti na Maulid Kitenge ambaye alitua wiki iliyopita akitokea EFM.

Wasafi Media inayomilikiwa na Msanii Nassibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ ipo katika mkakati wa  kujiimarisha na kuanza vipindi kwa saa 24 kuanzia wiki ijayo, huku tayari baadhi ya vipindi ikiwemo Sports Arena, Sports Court na Block 89 vikiwa vimeanza kuruka na kujipatia mashabiki.

Taarifa kutoka Wasafi Media zinaeleza kuwa, majina makubwa zaidi katika tasnia ya habari yanatarajiwa kutangazwa kujiunga na kituo hicho kuanzia leo Jumatano mpaka Jumapili hii, wakati vipindi vyote vikitarajiwa kuanza kuruka kuanzia Jumatatu ijayo.

Baadhi ya wamiliki wa vyombo vya habari, wameingiwa na hofu kubwa ya kupoteza watangazaji wao mahiri katika usajili mkubwa unaoendelea kufanywa na kituo cha Wasafi Media huku wananchi wengi wakiwa na kiu ya kuona ubora wa vipindi vya kituo hicho.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

Michezo

Usiku wa Ulaya umerejea kibabe kabisa

Spread the love  LIGI ya Mabingwa barani Ulaya imerejea tena na awamu...

Habari MchanganyikoMichezo

Mambo ya Ndani, Ulinzi zang’ara michezo ya Mei Mosi Arusha

Spread the loveRais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi nchini (TUCTA), Tumaini...

Michezo

Beti na Meridianbet mechi za leo

Spread the love IKIWA leo hii ni Jumapili tulivu kabisa, Meridianbet wanamkwambia...

error: Content is protected !!