Saturday , 3 June 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Ukipanda chuki, utavuna chuki – Zitto
Habari za Siasa

Ukipanda chuki, utavuna chuki – Zitto

Zitto Kabwe, Kiongozi Mkuu wa ACT-Wazalendo
Spread the love

ZITTO Kabwe, Kiongozi Mkuu wa Chama cha ACT-Wazalendo, amesema nchi imevimba usaa wa chuki. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Zitto ametoa kauli hiyo tarehe 22 Oktoba 2019, wakati akizungumza na wanahabari jijini Dar es Salaam.

“Ukijenga matumaini kwa nchi, unavuna vitu vingi, lakini ukipanda chuki, utavuna chuki. Viongozi wajue nchi imevimba usaa wa chuki, wanawajibu wa kutumbua usaha wa chuki uliotunga kwenye nchi yetu,” amesema Zitto. 

Kiongozi huyo ambaye ni mbunge wa Kigoma Mjini amesema, nchi inapitia katika kipindi kigumu, ambacho baadhi ya watu wamefikia hatua ya kufurahia matatizo yanayowapata wenzao wenzao.

Amewataka viongozi kuiondoa hiyo chuki ili Taifa lirudi katika umoja na mshikamano.

“Tuwe na amani, tujibizane, tuwe wamoja tuendeelee kuwa kama watanzania. Ni wajibu wa viongozi kuondoa hiyo chuki ili tuwe wamoja. Mbele ya Mungu hakuna mtu aliyechuma wote ni udongo na tutarudi kwa udongo,” ameeleza Zitto.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Lusinde: CCM hatuliachii ng’o jimbo la Moshi Mjini

Spread the loveMJUMBE wa Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi (NEC), Livingston...

Habari za SiasaTangulizi

Serikali ya Mapinduzi Zanzibar: Bakharesa hajavamia shamba letu

Spread the love  IKULU Visiwani Zanzibar, imeeleza kuwa eneo la kiwanda cha...

Habari za SiasaTangulizi

Zanzibar watangaza rasmi kuwa shamba la Razaba ni mali yao

Spread the love  SERIKALI ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), imetangaza rasmi kwamba shamba...

Habari za SiasaTangulizi

Rais Mwinyi azindua Kamati ya Maridhiano Visiwani

Spread the love  RAIS wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), Dk. Hussein...

error: Content is protected !!