Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Magufuli aagiza wanaochunguza masuala nyeti walindwe
Habari za Siasa

Rais Magufuli aagiza wanaochunguza masuala nyeti walindwe

Spread the love

RAIS John Magufuli ameagiza vyombo vya dola kulinda watumishi wa Ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali wanaochunguza masuala mazito, ili wasiingiliwe katika utekelezaji wa majukumu yao. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Gerson Msigwa, Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, Rais Magufuli ametoa agizo hilo leo tarehe 20 Agosti 2019 alipotembelea ofisi hiyo iliyoko jijini Dar es Salaam, kwa ajili ya kuangalia utendaji kazi wake.

Taarifa hiyo imeeleza kuwa, Rais Magufuli amevitaka vyombo vya ulinzi na usalama kuhakikisha watumishi hao wanakuwa salama na hawaingiliwi kwenye majukumu yao.

Wakati huo huo, Rais Magufuli amewataka wafanyakazi wa Mamlaka ya Mkemia Mkuu wa Serikali kufanya kazi kwa uadilifu pasina kujihusisha na vitendo vya rushwa pamoja na kutoa siri za wateja wao.

Katika ziara yake hiyo,  Rais Magufuli amejionea namna mitambo ya uchunguzi wa kisasa ya ofisi hiyo inavyofanya kazi ikiwemo kuchunguza vinasaba vya miili ya watu waliopoteza maisha katika ajali ya moto mkoani Morogoro, iliyotokea hivi karibuni.

“Katika maabara hiyo, Rais Magufuli amejionea mitambo mipya ya uchunguzi wa vinasaba vya binadamu, sumu, dawa za kulevya na kemikali,” inaeleza taarifa ya Msigwa.

Aidha, Rais Magufuli amemuagiza Profesa Ester Jason, Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka hiyo na Dk. Fidelis Mafumiko, Mkemia Mkuu wa Serikali, kusimamia vizuri matumizi ya fedha za kununulia mahitaji mbalimbali ikiwemo vitenganishi vya maabara.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

error: Content is protected !!