Friday , 29 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Mkemia Mkuu atambua miili 50 ajali ya Moro
Habari Mchanganyiko

Mkemia Mkuu atambua miili 50 ajali ya Moro

Lori la mafuta likiteketea kwa moto na kusababisha baadhi ya watu kuungua moto
Spread the love

OFISI ya Mkemia Mkuu wa Serikali imefanikiwa kutambua miili 50 kati ya 69 ya watu waliopoteza maisha katika ajali ya moto wa lori la mafuta mkoani Morogoro.  Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Taarifa hiyo imetolewa jana tarehe 20 Agosti 2019 na Gerson Msigwa, Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu wakati akizungumzia ziara ya Rais John Magufuli katika ofisi hiyo iliyoko jijini Dar es Salaam.

Akizungumza katika ziara hiyo, Rais Magufuli ametoa wito kwa ndugu kujitokeza ili wachukuliwe sampuli zao kwa ajili ya kutambua miili ya ndugu zao mahala ilipozikwa.

Aidha, Rais Magufuli ameitaka ofisi hiyo kuendelea kutoa taarifa kwa umma ili ziwafikie walengwa kitendo kitakachosaidia kupata ndugu wa miili 19 iliyobakia.

“Wale wengine kama alivyotoa wito  kiongozo wenu basi kama kuna ndugu wanaweza kuwa tayari wapimwe, ili pawepo ‘comparison’ ya marehemu wachache waliobakia. Mmefanya kazi kubwa sana na hizi taarifa mzitoe mapema mzitangaze sababu itasaidia ndugu wa marehemu kupimwa,” amesema Rais Magufuli.

Wakati huo huo, Rais Magufuli amewaomba Watanzania kuwaombea kwa Mungu majeruhi wa ajali hiyo wanaopatiwa matibabu katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) na Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Morogoro, ili wapone haraka na waungane na familia zao.

“Lakini wale walioko kule tuendelee kuwaombea Mungu awasaidie, kikubwa ninachotaka kusema ni kwamba ofisi yenu ya mkemia mkuu na ninyi wakemia mmefanya kazi kubwa sana ninawapongeza sana,” amesema Rais Magufuli.

Ajali ya moto wa lori la mafuta ilitokea tarehe 10 Agosti mwaka huu mkoani Morogoro, ambapo mpaka sasa imepoteza maisha ya watu zaidi ya 90.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoKimataifa

Zuma akataliwa kugombea urais

Spread the loveTUME Huru ya Uchaguzi Afrika Kusini (IEC) imemwondoa rais wa...

Habari Mchanganyiko

Mtandao watetezi wa haki za mazingira Tanzania waundwa

Spread the loveMTANDAO wa watetezi wa haki za mazingira nchini Tanzania, umeundwa...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga kuongoza usambazaji wa mitungi ya gesi 10,000 ya Taifa Gas

Spread the loveNaibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga ameahidi kuongoza kwa ufanisi...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyabiashara, wawekezaji China waridhia kuwekeza bil. 800 katika sekta 5 nchini

Spread the loveUJUMBE wa wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa kutoka Jimbo la Changzhou...

error: Content is protected !!