Sunday , 5 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Kabendera kupandishwa kizimbani
Habari Mchanganyiko

Kabendera kupandishwa kizimbani

Erick Kabendera
Spread the love

MWANDISHI wa Habari, Erick Kabendera kesho tarehe 1 Agosti 2019 anatarajiwa kupandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Kabendera anayetuhumiwa kuwa sio raia wa Tanzania, atapandishwa kizimbani hapo kesho majira ya saa tatu asubuhi. Baada ya Mtandao wa Kutetea Haki za Binadamu (THRDC) kupitia mawakili wake, kufungua maombi ya dhamana Namba 14 ya mwaka 2019.

Kabendera anatetewa na Mawakili Jones Sendodo, Shilinde Swedy na Catherine Ringo kutoka mtandao wa THRDC.

Loy Kabendera mke wa Kabendera leo tarehe 31 Julai 2019 ameruhusiwa kumuona mume wake ikiwa zimepita siku mbili tangu alipokamatwa na jeshi la Polisi tarehe 29 Julai mwaka huu, akiwa nyumbani kwake Mbweni Jijini Dar es salaaam.

Kwa mujibu wa THRDC, Kanbendera anashikiliwa katika Kituo cha Polisi cha Kilwa Road.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoTangulizi

Kimbunga Hidaya chatikisa Mafia

Spread the loveWAKATI hali ya upepo mkali ikiendelea kushuhudiwa katika baadhi ya...

Habari MchanganyikoTangulizi

Usafiri baharini wasitishwa kukwepa athari za kimbunga Hidaya

Spread the loveUSAFIRI wa baharini umesimamishwa kwa muda ili kukwepa athari za...

Habari Mchanganyiko

RPC Dodoma akabidhiwa bunduki mbili za wahalifu

Spread the love  Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa ya Kulevya...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC yazindua huduma maalum kwa wastaafu

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) imezindua huduma maalum kwa...

error: Content is protected !!