Friday , 29 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Kabendera kupandishwa kizimbani
Habari Mchanganyiko

Kabendera kupandishwa kizimbani

Erick Kabendera
Spread the love

MWANDISHI wa Habari, Erick Kabendera kesho tarehe 1 Agosti 2019 anatarajiwa kupandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Kabendera anayetuhumiwa kuwa sio raia wa Tanzania, atapandishwa kizimbani hapo kesho majira ya saa tatu asubuhi. Baada ya Mtandao wa Kutetea Haki za Binadamu (THRDC) kupitia mawakili wake, kufungua maombi ya dhamana Namba 14 ya mwaka 2019.

Kabendera anatetewa na Mawakili Jones Sendodo, Shilinde Swedy na Catherine Ringo kutoka mtandao wa THRDC.

Loy Kabendera mke wa Kabendera leo tarehe 31 Julai 2019 ameruhusiwa kumuona mume wake ikiwa zimepita siku mbili tangu alipokamatwa na jeshi la Polisi tarehe 29 Julai mwaka huu, akiwa nyumbani kwake Mbweni Jijini Dar es salaaam.

Kwa mujibu wa THRDC, Kanbendera anashikiliwa katika Kituo cha Polisi cha Kilwa Road.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Mtandao watetezi wa haki za mazingira Tanzania waundwa

Spread the loveMTANDAO wa watetezi wa haki za mazingira nchini Tanzania, umeundwa...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga kuongoza usambazaji wa mitungi ya gesi 10,000 ya Taifa Gas

Spread the loveNaibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga ameahidi kuongoza kwa ufanisi...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyabiashara, wawekezaji China waridhia kuwekeza bil. 800 katika sekta 5 nchini

Spread the loveUJUMBE wa wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa kutoka Jimbo la Changzhou...

Habari Mchanganyiko

Bil. 4.42 kumaliza uhaba maji kata 2 Musoma Vijijini

Spread the loveWANANCHI wa kata za Busambara na Kiriba, Jimbo la Musoma...

error: Content is protected !!